-
Iran: Tutajikita katika kuimarisha uhusiano na mataifa ya Afrika
Feb 22, 2025 08:33Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran imesisitiza kuwa, irada ya Jamhuri ya Kiislamu imeelekezwa katika kuimarisha uhusiano wake na mataifa ya Afrika.
-
Katibu Mkuu wa UN aahidi Afrika kuwa na mwakilishi wa kudumu kwenye Baraza la Usalama
Feb 16, 2025 10:43Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema sio sawa kwa bara la Afrika kutokuwa na kiti cha mwakilishi wa kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na ameahidi kufanya kazi na Umoja wa Afrika na nchi wanachama ili kuhakikisha kuwa nchi za Afrika zinapata mwakilishi wa kudumu katika Baraza la Usalama.
-
Mtaalamu wa Zambia: Ushuru wa Trump utawadhuru zaidi Wamarekani
Feb 14, 2025 23:12Mtaalamu mmoja wa masuala ya biashara, ujasiriamali na uwezekaji wa Zambia amesema uamuzi wa serikali ya Marekani wa kutoza ushuru wa juu kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka Canada, Mexico, na China utawadhuru zaidi Wamarekani.
-
IOM: Vita vya Sudan vimeongeza idadi ya wakimbizi wa ndani Pembe ya Afrika
Feb 04, 2025 23:10Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limesema idadi ya wakimbizi wa ndani (IDP) katika Pembe ya Afrika iliongezeka hadi milioni 20.75 kufikia mwishoni mwa mwaka uliopita wa 2024.
-
Russia: Kwa mtazamo wa mkuu wa UNICEF watoto wa Ghaza si muhimu kama wenzao wa Ukraine
Jan 25, 2025 02:42Balozi wa Russia katika Umoja wa Mataifa amemshutumu mkuu wa UNICEF kwa kuwapa kipaumbele watoto wa Ukraine kuliko watoto wenzao wa Ghaza baada ya kushindwa kulieleza Baraza la Usalama la umoja huo kuhusu masaibu ya watoto hao kama alivyofanya kwa watoto wa Ukraine.
-
Nchi za Magharibi zina nafasi gani katika kuongezeka ugaidi Afrika?
Jan 22, 2025 23:18Kuongezeka kwa shughuli za kigaidi katika maeneo mbalimbali ya Afrika kumegeuka kuwa tatizo kubwa katika bara hilo na pia katika mataifa mengi duniani. Hivi sasa, makundi kadhaa ya kigaidi yanaendesha shughuli zao katika maeneo tofauti ya Afrika.
-
UN: Mapambano dhidi ya ugaidi barani Afrika yaheshimu haki za binadamu
Jan 22, 2025 10:03Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, mapambano ya kukabiliana kikamilifu na ugaidi barani Afrika yanapaswa kuhusisha uvumbuzi na mtazamo unaoheshimu haki za binadamu na utawala wa sheria.
-
Ghalibaf: Changamoto ya uhusiano wa kiuchumi wa Iran na Afrika ni usafiri
Jan 17, 2025 03:51Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ameyataja matatizo ya usafiri kuwa ni miongoni mwa changamoto kubwa katika kupanua uhusiano wa kiuchumi wa Iran na bara la Afrika akisema: Uwezo wa kimataifa kama wa kundi la BRICS na Shanghai ni fursa muhimu za kustawisha ushirikiano wa kiuchumi.
-
Viongozi wa Afrika wasisitiza ushirikiano katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi
Jan 16, 2025 07:36Viongozi wa nchi za Kiafrika wamesisitiza udharura wa kushirikiana nchi za bara hilo na kubuni tekolojia ya kukabiliana na athari mbaya za mabadiliko ya tabianchi ili kuhakikisha bara la Afrika linapata maendeleo endelevu.
-
Besigye kushtakiwa katika Mahakama ya Kijeshi Uganda kwa kosa la uhaini lenye hukumu ya kifo
Jan 14, 2025 23:16Mahakama ya Kijeshi ya Uganda imetangaza kuwa, kiongozi mashuhuri wa upinzani nchini humo Daktari Kizza Besigye atafikishwa mahakamani kujibu shtaka zito la uhaini, ambalo linamuongezea matatizo ya kisheria mwanasiasa huyo kuelekea uchaguzi wa rais uliopangwa kufanyika 2026.