-
Askari wa Uganda waua magaidi 22 wa Al-Shabaab nchini Somalia
Apr 02, 2018 03:09Jeshi la Uganda UPDF limesema askari wake walio katika Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika Somalia, AMISOM, wamewaua magaidi 22 wa kundi la al-Shabab.
-
Al Shabab yashambulia kambi ya Umoja wa Afrika karibu na Mogadishu
Apr 01, 2018 12:54Wanamgambo wa kundi la al Shabab leo wamepigana kwa masaa kadhaa na wanajeshi wa Umoja wa Afrika baada ya kulipua gari walilotega bomu ndani yake nje ya kambi ya wanajeshi hao.
-
Askari 5 wa AU miongoni mwa watu 16 waliouawa katika hujuma za al-Shabaab Somalia
Mar 04, 2018 04:46Imerifiwa kuwa, wanajeshi watano wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia Amisom ni miongoni mwa watu 16 waliouawa katika mashambulizi ya hivi karibuni ya kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab karibu na Mogadishu.
-
Al-Shabaab yaua askari polisi 5 wa Kenya kaunti ya Mandera
Mar 02, 2018 04:24Askari polisi watano wa Kenya wameuawa na wengine watatu kujeruhiwa baada ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab kushambulia kambi mbili za maafisa usalama katika mji wa Fino katika kaunti ya Mandera.
-
Amisom: Tumekomboa 80% ya maeneo yaliyokuwa chini ya al-Shabaab Somalia
Mar 02, 2018 04:13Kikosi cha Kusimamia Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia Amisom kimesema kimefanikiwa kukomboa asilimia 80 ya maeneo ambayo yalikuwa kwenye makucha ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab.
-
Serikali ya Kenya yaahidi kukomesha ugaidi unaovuruga elimu
Feb 28, 2018 13:00Serikali ya Kenya imetangaza kuwa imebuni mpango ambao utahakikisha kwamba shughuli za masomo hazitaathiriwa katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa nchi hiyo hususan katika Kaunti ya Wajir kutokana na mashambulizi ya kigaidi ya kundi la al Shabab.
-
UN yasema itaendelea kuunga mkono mapambano dhidi ya al-Shabaab Somalia
Feb 25, 2018 11:59Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa sambamba na kulaani mashambulizi ya kigaidi ya hivi karibuni yaliyoua makumi ya watu katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu, amesisitiza kuwa umoja huo utaendelea kuunga mkono jitihada za kulitokomeza kundi la kigaidi na la ukufurishaji la al-Shabaab.
-
Magaidi wanne watiwa mbaroni katikati ya Somalia
Feb 08, 2018 00:29Jeshi la Somalia limetangaza habari ya kutiwa mbaroni magaidi wanne wa genge la wakufurishaji la al Shabab, katikati ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Jeshi la Somalia laukomboa mji uliokuwa ukishikiliwa na Al Shabab
Jan 20, 2018 01:08Jeshi la Somalia limeukomboa mji wa kusini wa Bar-Sanguni uliokuwa ukishikiliwa na kundia la magaidi wakufurishaji wa Al-Shabaab, na kuwaua wapiganaji saba wa kundi hilo, wakiwemo makamanda wake wanne waandamizi.
-
Makumi ya watoto waokolewa kutoka shule ya al-Shabaab Somalia
Jan 19, 2018 10:16Serikali ya Somalia imesema askari wa nchi hiyo wamevamia shule iliyokuwa ikiendeshwa na kundi la kigaidi la al-Shabaab na kuokoa makumi ya watoto toka kwenye makucha ya genge hilo la ukufurishaji.