-
Kiongozi wa Boko Haram aibuka, adai wamehusika katika mashambulizi
Jan 02, 2018 15:00Kiongozi wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram, Abubakar Shekau ametoa kanda mpya ya video na kudai kuwa kundi hilo ndilo lililohusika na wimbi la mashambulizi ya bomu katika sherehe za kufunga mwaka, kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Boko Haram yaua watu watatu nchini Cameroon
Dec 24, 2017 15:40Duru za kieneo zimetangaza kuwa watu wasiopungua watatu wameuawa katika shambulio la kigaidi la kundi la wakufurishaji la Boko Haram, kaskazini mwa Cameroon.
-
Jeshi la Nigeria laua wanamgambo 20 wa kundi la kigaidi la Boko Haram
Dec 20, 2017 16:19Jeshi la Nigeria limetangaza leo kuwa limewaua wanamgambo 20 wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram katika operesheni linazoendelea kufanya ili kutokomeza mabaki ya magaidi hao.
-
Vita dhidi ya Boko Haram vyazidi kuungwa mkono nchni Nigeria
Dec 15, 2017 04:15Wakuu wa mikoa tofauti ya Nigeria jana walikubaliana na mpango wa kutenga kitita cha dola bilioni moja kwa ajili ya kuisaidia Serikali Kuu kupambana na genge la kigaidi la Boko Haram.
-
Watu watano wauawa na wanamgambo wa Boko Haram Nigeria
Dec 14, 2017 07:42Watu wasiopungua watano wameuawa katika shambulio la hivi kkaribuni kabisa la wanamgambo wa Boko Haram nchini Nigeria kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
Boko Haram waua watu wasiopungua 13 katika jimbo la Borno nchini Nigeria
Dec 02, 2017 15:05Washambuliaji wa kujitoa mhanga wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram wamewaua watu wasiopungua 13 katika shambulio walilofanya leo kwenye soko moja katika mji wa Biu ulioko katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.
-
Kamanda wa Boko Haram atiwa mbaroni, wenzake 4 wauawa, mateka 212 wakombolewa
Nov 30, 2017 03:25Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa, limewakomboa raia wengine 212 waliokuwa wakishikiliwa mateka na wanachama wa kundi la kigaidi la Boko Haram katika msitu wa Sambisa.
-
Boko Haram waua wanajeshi watatu kaskazini mashariki mwa Nigeria
Nov 27, 2017 15:03Duru za usalama za Nigeria zimetangaza habari ya kuuawa wanajeshi watatu katika shambulizi la kigaidi lililofanywa na kundi la Boko Haram katika mji wa Magumeri, wa jimbo la Borno la kaskazini mashariki mwa nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.
-
Boko Haram yatwaa mji katika jimbo la Borno
Nov 26, 2017 07:53Kundi la kigaidi la Boko Haram limeutwaa mji mmoja katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria. Wakazi wa mji wa Magumeri wamesema kuwa magaidi wa kitakfiri jana waliingia katika mji huo yapata umbali wa kilomita 50 kutoka makao makuu ya Maiduguri.
-
Kuuliwa Waislamu msikitini katika shambulio la bomu la kujitoa mhanga nchini Nigeria
Nov 22, 2017 07:53Watu wasiopungua 50 wameaga dunia katika mlipuko wa bomu uliotokea msikitini kaskazini mashariki mwa Nigeria.