-
China yaonya kuhusu mripuko wa homa ya mapafu iliyo hatari zaidi ya Covid-19 Kazakhstan
Jul 10, 2020 03:38Ubalozi wa China nchini Kazakhstan umetoa indhari juu ya mripuko wa homa ya mapafu isiyojulikana (pneumonia) na ambayo ni hatari zaidi kuliko ugonjwa wa Covid-19.
-
Kujiondoa rasmi Marekani katika Shirika la Afya Duniani WHO
Jul 09, 2020 04:51Msimamo wa serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani ni kupuuza, kukosoa, kutoa vitisho na hatimaye kujitoa katika mashirika ya kimataifa na hasa yale yanayopinga matakwa na maslahi haramu ya nchi hiyo na ya washirika wake na hasa utawala haramu wa Israel.
-
Mousavi: Viongozi wa Iran na China wameazimia kustawisha uhusiano wa kistratejia
Jul 08, 2020 19:42Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa kwa mujibu wa mapatano ya mwaka 2016 kati ya Marais wa Iran na China, nchi mbili ziliweka wazi irada na azma yao ya kisiasa ya kustawisha na kupanua zaidi ushrikiano wa kistratejia na kuandaa ramani ya njia ya miaka 25 kati ya Tehran na Beijing ili kutayarisha uwanja mzuri wa ustawi wa pande zote katika uhusiano wa kisiasa na kiuchumi katika miaka ijayo.
-
China: Uvamizi na uhasama dhidi ya Palestina haupaswi kuhalalishwa
Jul 07, 2020 03:08Waziri wa Mambo ya Nje wa China ameashiria kuhusu uungaji mkono wa nchi hiyo ya Asia kwa wananchi madhulumu wa Palestina na kusisitiza kuwa, kuhujumiwa haki za msingi za Wapalestina hakupaswi kuhalalishwa.
-
Jitihada za Marekani za kuishawishi Ulaya iungane na Washington dhidi ya China
Jun 27, 2020 22:03Marekani katika kipindi cha utawala wa Rais Donald Trump imezididisha mienendo yake ya kukabiliana na China katika nyuga mbalimbali. Mbali na kutaka kuitwisha Beijing matakwa yake katika nyanja za kibiashara na kiuchumi, sasa Marekani inaingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo hususan katika maeneo mawili ya Hong Kong na Xinjiang kwa kisingizio cha haki za binadamu.
-
Njama za Marekani za kurefusha vikwazo vya silaha dhidi ya Iran kupitia Baraza la Usalama la UN
Jun 25, 2020 22:02Marekani imeanzisha kampeni kubwa za kimataifa za kulizuia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lisitekeleze azimio lake nambari 2231 linalotoa amri ya kuiondolea Iran vikwazo vya silaha ifikapo tarehe 18 Oktoba mwaka huu wa 2020. Marekani inaendesha njama hizo kama sehemu ya kukabiliana na uwezo mkubwa wa kiulinzi na kijeshi wa Iran unaozidi kukua na kuwa imara siku baada ya siku.
-
China yasema mashinikizo ya Marekani dhidi ya Iran hayatafika popote
Jun 24, 2020 03:51Balozi wa China katika Umoja wa Mataifa amesema mashinikizo ya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hayatafika popote.
-
Russia na China zakosoa azimio la Bodi ya Magavana ya IAEA dhidi ya Iran
Jun 19, 2020 23:37Russia na China zimekosoa hatua ya kupasishwa azimio dhidi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Trump aiomba China imsaidie kushinda uchaguzi mkuu ujao
Jun 18, 2020 04:01Mshauri wa zamani wa usalama wa taifa wa Marekani, John Bolton amesema katika kitabu chake kipya kwamba Rais Donald Trump wa nchi hiyo aliiomba China imsaidie katika kushinda uchaguzi mkuu wa rais uliopangwa kufanyika baadaye mwaka huu.
-
China yaionya India baada ya New Delhi kudai wanajeshi wake 20 wameuliwa na wanajeshi wa China mpakani
Jun 17, 2020 01:56Msemaji wa Jeshi la China ametoa onyo kali kwa India kuhusu vitendo vyake vya kichokozi katika eneo la mpaka wa nchi hizo mbili.