-
WFP: Matibabu ya utapiamlo yasitishwa nchini Ethiopia kutokana na ukosefu wa fedha
Apr 23, 2025 02:09Mpango wa Chakula Duniani (WFP) wiki hii umesimamisha matibabu ya utapiamlo kwa wanawake na watoto 650,000 nchini Ethiopia kutokana na uhaba mkubwa wa fedha. WFP imesema kuwa mamilioni ya watu wako katika hatari ya kukosa misaada.
-
Mamia ya waasi wa Fano wauawa katika operesheni ya jeshi la Ethiopia
Mar 23, 2025 02:40Wanajeshi wa Ethiopia wamewaua zaidi ya wapiganaji 300 wa kundi lenye silaha la Fano, washirika wao wa zamani dhidi ya waasi katika eneo la Tigray, katika siku mbili za mapigano mapya katika eneo la kaskazini la Amhara.
-
MSF yatahadharisha kuhusu kasi kipindupindu Ethiopia; watu 31 wameaga dunia
Mar 15, 2025 02:24Takriban watu 31 wapoteza maisha kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu unaoenea kwa kasi nchini Ethiopia.
-
Wavuvi 20 wa Kenya wauawa na wanamgambo wa Dassanech mpakani na Ethiopia
Feb 23, 2025 12:26Zaidi ya wavuvi 20 wameuawa katika eneo la mpaka la Todonyang, kaskazini mwa Kenya, pambizoni mwa Ziwa Turkana katika shambulio la watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Dassanech kutoka nchi jirani ya Ethiopia.
-
Mashauriano ya Iran na Ethiopia ya kupanua uhusiano wa kiuchumi
Jan 19, 2025 06:02Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia masuala ya Bunge amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mshauri katika Wizara ya Masuala ya Kigeni ya Ethiopia ambapo wamejadiliana njia za kupanua ushirikiano wa kiuchumi baina ya nchi hizi mbili ikiwemo uanachama katika kundi la "BRICS".
-
Spika wa Bunge la Iran awasili Ethiopia kwa ziara rasmi
Jan 17, 2025 03:20Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amewasili Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia akiongoza ujumbe wa ngazi za juu Bunge kwa mwaliko wa Spika wa Baraza la Wawakilishi la Ethiopia.
-
Juhudi za uokoaji zinaendelea Ethiopia baada ya kuathiriwa na tetemeko la ardhi
Jan 05, 2025 07:58Zeozi la kuwahamisha watu linaendelea huko Abomsa katikati mwa Ethiopia kufautia tetemeko la ardhi lililokuwa na ukubwa wa 5.8 kwa kipimo cha rishta kulikumba eneo hilo.
-
Ethiopia na Somalia zakubaliana kushirikiana katika kudumisha amani
Jan 03, 2025 12:03Ethiopia na Somalia zimekubaliana kufanya kazi pamoja katika kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AUSSOOM).
-
Watu 71 wafariki dunia baada ya basi la sherehe ya harusi kutumbukia mtoni nchini Ethiopia
Dec 30, 2024 12:21Takriban watu 71 wamepoteza maisha nchini Ethiopia baada ya basi lililokuwa limebeba abiria lililpoacha njia na kutumbukia mtoni. Haya yameelezwa na msemaji wa serikali ya jimbo la Sidama kusini mwa Ethiopia.
-
Watu milioni 7.3 waugua Malaria Ethiopia; 1,157 waaga dunia katika miezi 9
Nov 15, 2024 07:43Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, watu zaidi ya milioni 7.3 wamepatwa na ugonjwa wa Malaria nchini Ethiopia huku wagonjwa 1,157 wakiaga dunia kwa ugonjwa huo kuanzia Januari Mosi hadi Oktoba 20 mwaka huu.