-
Hamas yapinga makubaliano yanayotambua rasmi uwepo wa Israel huko Ghaza
Sep 06, 2024 07:26Mkuu wa timu ya mazungumzo ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, amesema harakati hiyo ya muqawama haitaafiki makubaliano ambayo yanahalalisha uwepo wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Ghaza.
-
Kuunga mkono Iran maamuzi ya wananchi na muqawama wa Palestina
Sep 04, 2024 12:41Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza kuwa, Tehran inaunga mkono makubaliano na uamuzi wowote wa makundi ya muqawama na wananchi wa Palestina.
-
Yemen wafanya maandamano ya mamilioni ya watu kuwaunga mkono Wapalestina
Aug 31, 2024 04:15Kwa mara nyingine tena mamilioni ya wananchi wa Yemen wamemiminika barabarani kulaani jinai za utawala wa Kizayuni na kuwaunga mkono wananchi wa Palestina hasa wa Ukanda wa Ghaza.
-
UN: Mripuko mpya wa Kipindupindu Sudan unahatarisha maisha ya mamia ya maelfu ya wakimbizi
Aug 24, 2024 09:54Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limeeleza kupitia mwakilishi wake nchini Sudan Kristine Hambrouck kwamba mripuko mpya wa kipindupindu nchini Sudan, ambao ni wimbi la pili tangu vilipoanza vita miezi kumi na sita iliyopita, unahatarisha maisha ya jamii zilizolazimika kuyahama makazi yao nchini kote.
-
Askari 695 wa Israel wameangamizwa, 4,357 wamejeruhiwa tangu vilipoanza vita vya Ghaza
Aug 24, 2024 02:34Msemaji wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel ametangaza kuwa askari 695 wa utawala huo wameangamizwa tangu jeshi la utawala huo katili lilipoanzisha vita dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Ghaza na kupambana na vikosi vya Muqawama wa Palestina.
-
Ombi la Shirika la Haki za Binadamu la Ulaya-Mediterranean la kuwekewa vikwazo Israel
Aug 22, 2024 10:46Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Ulaya na Mediterania (The Euro-Mediterranean Human Rights Monitor-Euro-Med-) limeonya katika taarifa yake siku ya Jumatano kuhusu amri za mara kwa mara za utawala wa Kizayuni wa Israel za kuwataka Wapalestina wahame katika maeneo tofauti ya Gaza na kuzitaka nchi za dunia ziuwekee vikwazo utawala huo ghasibu na zisiuunge mkono.
-
Takwa la Waislamu wa Marekani kwa Biden la kulaani ugaidi wa kiserikali wa Israel
Aug 11, 2024 13:40Baraza la Mahusiano ya Kiislamu Marekani (CAIR) limemtaka Rais Joe Biden wa nchi hiyo ajibu na kulaani vitendo vya ugaidi wa kiserikali vinavyofanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran: Taasisi za kimataifa ni washirika katika jinai za utawala wa Kizayuni
Aug 11, 2024 11:27Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa taasisi za kimataifa zinashiriki katika jinai za utawala wa Kizayuni.
-
Maandamano ya kulaani jinai za Israel yaendelea kufanyika nchini Morocco
Aug 10, 2024 02:32Maelfu ya wananchi wa Morocco wamefanya maandamano katika miji mbalimbali ya nchi hiyo kuwaunga mkono wananchi wa Palestina na kulaani jinai zinazoendelea kufanywa na jeshi la Israel huko Gaza.
-
Ripoti: Israel imeiba zaidi ya miili 2,000 kutoka kwenye makaburi ya Gaza
Aug 06, 2024 12:16Vikosi vya jeshi la Israel vimeiba zaidi ya miili 2,000 iliyofukuliwa kutoka kwenye makaburi mbalimbali katika ukanda wa Gaza, huku ripoti kutoka Ofisi ya Vyombo vya Habari ya Serikali ya Gaza zikisema baadhi ya maiti zimerudishwa baada ya majeshi ya Israel "kuvunjia heshima miili" ya marehemu hao.