-
UN yaunga mkono maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu Marekani ya kuwatetea watu wa Gaza
Apr 28, 2024 04:26Stephen Dujaric Msemaji wa Umoja wa Mataifa jana Ijumaa alisema katika radiamali yake kwa maandamano yanayoendelea kufanywa na wanafunzi wa vyuo vikuu huko Marekani katika kuwaunga mkono watu wa Gaza na kupinga mauaji ya kimbari dhidi ya wakazi wa eneo hilo kwamba: Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ni mfuasi na mungaji mkono mkubwa wa uhuru wa kujieleza, ikiwa ni pamoja na huko Marekani; na anaunga mkono haki ya wananchi ya kufanya maandamano kwa amani.
-
Wachambuzi: Maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu Marekani yanamuweka Biden matatani
Apr 27, 2024 11:44Duara la maandamano ya wanafunzi wa vyuo viku dhidi ya vita vya Israel katika Ukanda wa Gaza linazidi kupanuka nchini Marekani, na kusababisha mkanganyiko mkubwa katika hesabu za Israel na waungaji mkono wake.
-
Mbali na walionyofolewa viungo, Wapalestina wengine walizikwa wakiwa hai kwenye makaburi ya halaiki Ghaza
Apr 27, 2024 02:47Wahudumu wa afya, timu za uokoaji na mashirika ya kutetea haki za binadamu yanawashutumu askari vamizi wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuwanyofoa viungo Wapalestina na hata kuwazika baadhi yao wakiwa hai kwenye makaburi ya halaiki yaliyogunguliwa kwenye eneo la karibu na Hospitali ya Nasser huko Ukanda wa Ghaza, baada ya askari hao katili kuondoka katika eneo hilo Aprili 7 kufuatia mashambulizi ya ardhini ya miezi minne.
-
Hizbullah: Tumeua na kujeruhi askari 2,000 wa Israel katika operesheni 1,650 tangu vilipoanza vita vya Ghaza
Apr 25, 2024 12:16Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imesema imeua na kujeruhi zaidi ya wanajeshi 2,000 wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika operesheni zake 1,650 ilizotekeleza katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu tangu kuanza kwa vita vya mauaji ya kimbari vya utawala huo katika Ukanda wa Ghaza.
-
Kwa mara ya kwanza, Hizbullah yashambulia ndani kabisa ya ngome za Wazayuni tangu vilipoanza vita vya Ghaza
Apr 24, 2024 02:44Hizbullah ya Lebanon imetangaza kuwa imefanya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani dhidi ya vituo viwili vya kiejshi vya utawala wa Kizayuni wa Israel kulipiza kisasi cha mauaji ya wapiganaji wake wawili.
-
Kamishna wa UN: Picha ya mtoto anayetolewa kwenye fuko la mama yake anayekata roho Ghaza ni zaidi ya tukio la vita
Apr 24, 2024 02:44Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amekemea vikali mashambulio ya kinyama na ya mfululizo yaliyofanywa hivi karibuni na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda Gaza na kuua zaidi wanawake na watoto.
-
Kujitetea kwerevu kwa Iran kwa ajili ya Gaza
Apr 17, 2024 11:41Hatua ya Iran kujitetea kihalali dhidi ya shambulio la kichokozi la utawala wa Kizayuni katika ubalozi mdogo wake nchini Syria, ambayo ilifanyika kwa utaratibu wa hali ya juu na kupitia silaha tofauti za mashambulio, imekuwa na athari na matokeo ya kieneo na kimataifa angalau imepelekea wakaazi wa Gaza kupata usiku mmoja wa amani na utulivu.
-
Rais wa Uturuki: Israel imempiku Hitler kwa kuua watoto 14,000 wasio na hatia Ghaza
Apr 17, 2024 11:11Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amesema, Israel tayari imempiku kiongozi wa Wanazi Adolf Hitler kwa kuua zaidi ya watoto 14,000 wasio na hatia katika Ukanda wa Ghaza.
-
Katika barua kwa Papa, Erdogan ataka Ubinadamu ukomeshe ukiukaji zaidi wa sheria unaofanywa Ghaza
Apr 14, 2024 02:32Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki ametoa wito kwa watu duniani kote kuzungumza dhidi ya mashambulizi ya kinyama ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya hospitali, skuli, misikiti na makanisa katika Ukanda wa Ghaza, Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
UNICEF: Watoto wa Ghaza wako taabani kwa kula nyasi
Apr 13, 2024 02:15Msemaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF amesema, ameshuhudia kwa macho yake mtoto aliye taabani baada ya kula nyasi kutokana na njaa inayokabili mamia ya maelfu ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.