-
The Guardian: Imarati imempatia Haftari tani 5,000 za silaha
Mar 12, 2020 23:20Ripoti iliyoandikwa na gazeti la Guardian la Uingereza imefichua kuwa, nchi ya Umoja wa Falme wa Kiarabu (Imarati) imempatia jenerali mstaafu wa Libya, Khalifa Haftar tani elfu tano za silaha tangu mwezi Januari mwaka huu.
-
Mkuu wa Jumuiya ya kimataifa ya Maulamaa wa Kiislamu: Imarati inaeneza chuki na uharibifu duniani
Feb 28, 2020 23:12Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Wanazuoni wa Kiislamu ameishambulia vikali Imarati akiituhumu kuwa inaeneza vita, njama na vinyongo katika pembe mbalimbali za dunia.
-
Imarati yawatumia wapiganaji wa Haftar ndege 100 zilizosheheni silaha
Feb 25, 2020 04:30Imebainika kuwa, ndege 100 za mizigo zilizosheheni silaha na zana za kijeshi zimewasili nchini Libya zikitokea Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati).
-
Vijana wa Sudan wasimulia jinsi Abu Dhabi ilivyowapeleka kupigana vita Libya
Feb 15, 2020 23:21Vijana wa Kisudan waliorejea makwao hivi karibuni wamesimulia jinsi walivyohadaiwa na kampuni ya Black Shield Security Services iliyowaahaidi kuwapa kazi za ulinzi na badala yake walijikuta wakipewa mafunzo ya kijeshi yasiyooana na kazi zao na kupelekwa bila ya kujua huko Libya na Yemen kupigana vita.
-
Maafisa wa Imarati wafunguliwa mashtaka ya kufanya uhalifu wa kivita huko Yemen
Feb 13, 2020 07:58Shirika moja la mawakili la Uingereza limefungua mashtaka dhidi ya maafisa wa serikali ya Imarati kwa tuhuma za kutenda jinai za kivita nchini Yemen.
-
Ripoti ya Independent: Kengele za vita zasikika zaidi katika milango ya Libya
Jan 29, 2020 11:35Ripoti iliyotolewa na gazeti la Independent la Uingereza imefichua kuwa, mapatano tete ya kusitisha vita yaliyofikiwa hivi karibuni baina ya madola makubwa mjini Berlin huko Ujerumani yanaelekea kuporomoka kutokana na mashambulizi ya anga yanayoshuhudiwa sasa nchini Libya na vitisho vinavyoendelea kutolewa na pande hasimu.
-
Kirusi cha Corona chafika Imarati, Taiwan na Sudan, idadi ya waliofariki dunia inaongezeka
Jan 29, 2020 10:45Kirusi hatari cha Corona kimeripotiwa kufika katika nchi za Imarati na Taiwan huku idadi ya watu wanaofariki dunia na kuambukizwa kirusi hicho ikiongezeka kwa kasi.
-
Hamas yakosoa hatua ya Imarati kuialika Israel katika Maonyesho ya Dubai
Jan 21, 2020 03:57Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas imesema hatua ya Umoja wa Falme za Kiarabu ya kuualika utawala haramu wa Israel kushiriki katika Maonyesho ya Dubai ya 2020 ni aina fulani ya kuufanya wa kawaida uhusiano wa taifa hilo la Kiarabu na Tel Aviv.
-
Netanyahu apongeza juhudi za Imarati za kuimarisha uhusiano na Israel
Dec 22, 2019 10:33Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel amepongeza jitihada zinazofanywa na Umoja wa Falme za Kiarabu za kutaka kuimarisha na kufanya wa kawaida uhusiano wa utawala huo pandikizi na baadhi ya nchi za Kiarabu.
-
Fayez al Sarraj: Mashambulizi ya droni za Imarati hayatasalia bila jibu
Dec 22, 2019 03:23Fayez al Sarraj Waziri Mkuu wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya jana usiku alisema kuwa mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) za Imarati katika maeneo ya Zliten na Msalata kaskazini mwa nchi hiyo ni hatua ya kihalifu ambayo haitasalia bila ya jibu.