-
Kufichuliwa kushiriki maafisa wa kijeshi wa Marekani katika vita vya Saudia dhidi ya Yemen
Jun 14, 2018 05:04Kwa mujibu wa wa jarida la Ufaransa la Intelligence Online, Umoja wa Falme za Kiarabu, UAE, umewaajiri maafisa wa jeshi la Marekani waliostaafu ili waweze kuwasaidia wanajeshi wake katika vita dhidi ya Yemen. Imedokezwa kuwa, UAE imewaajiri mamluki hao ambao waliwahi kuhudumu katika ngazi mbali mbali katika Wizara ya Ulinzi ya Marekani, Pentagon.
-
Vikosi vya Yemen vyazima mashambulizi ya Saudia al-Hudaydah
Jun 14, 2018 03:38Jeshi la Yemen likishirikiana na vikosi vya kujitolewa vya wananchi limefanikiwa kuzima mashambulizi ya muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia, dhidi ya bandari ya al-Hudaydah ambayo ndilo lango kuu la kuingizia misaada ya kibinadamu kwa raia wanaoendelea kuua ovyo wa Yemen.
-
Watunisia waandamana kupinga njama chafu za Imarati dhidi ya nchi yao
Jun 13, 2018 21:54Raia wa Tunisia wamefanya maandamano wakipinga njama chafu na uingiliaji wa Imarati katika masuala ya ndani ya nchi yao.
-
Qatar yaishtaki Imarati katika mahakama ya haki za binadamu ya UN
Jun 12, 2018 09:20Qatar imewasilisha faili la kesi dhidi ya Umoja wa Falme za Kiarabu, katika mahakama ya juu zaidi ya Umoja wa Mataifa, ikiituhumu Abu Dhabi kwamba imekiuka haki za binadamu za wananchi wa Qatar, huku mgogoro wa nchi hizo za Kiarabu ukielekea kutimiza mwaka mmoja.
-
Utajiri wa Imarati (UAE) na Saudia unatumikia malengo ya Wazayuni
Jun 10, 2018 12:19Naibu wa Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Palestina katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu amesema, pesa za Imarati (UAE) na Saudi Arabia zinatumiwa kwenye mipango na njama za utawala ghasibu wa Israel kwa lengo la kununua milki za ardhi na majengo za Wapalestina kandokando ya msikiti wa Al-Aqsa.
-
Misri na Imarati zapinga kufanyika uchaguzi wa Rais na Bunge nchini Libya
Jun 09, 2018 22:19Misri na Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) zimeelezea kutofurahishwa kwao na maamuzi wa mkutano wa mjini Paris Ufaransa kuhusiana na Libya na kusema kuwa zinapinga uchaguzi wa Rais na Bunge uliopangwa kufanyika nchini humo tarehe 10 Disemba mwaka huu.
-
Ripoti: Saudia na Imarati zinapanga kufanya mapinduzi Bahrain
Jun 09, 2018 03:39Tovuti ya habari ya Middle East Eye imeripoti kuwa, Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu zinapanga njama ya kumuondoa mamlakani Waziri Mkuu wa Bahrain, Khalifa bin Salman Aal-Khalifah.
-
Oman yasema haiwezi kuvumilia tena chokochoko za UAE
Jun 08, 2018 20:53Migogoro inazidi kutokota katika Ghuba ya Uajemi baada ya Oman kuuonya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kuwa haiwezi kuvumilia tena wizi wa turathi zake za kitaifia na haki za uvumbuzi.
-
Imarati yakiri kwamba lilikuwa kosa kuiondoa Syria Arab League
Jun 07, 2018 02:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Imarati amekiri wazi kwamba maamuzi ya kuiondoa Syria katika Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) yalikuwa makosa makubwa.
-
Mwaka mmoja wa mgogoro kati ya nchi za Kiarabu
Jun 06, 2018 01:27Umetimia mwaka mmoja tokea uanze mgogoro baina ya nchi za Kiarabu na dalili zote zinaonyesha kuwa mgogoro huo ungali unaendelea bali hata utazidi kupanuka na kuwa mbaya zaidi.