-
Iran yasikitishwa na shambulio la kigaidi lililoua makumi Nigeria
Jun 07, 2022 03:39Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani shambulio la kigaidi lililoua makumi ya watu kanisani huko Nigeria hivi karibuni, sanjari na kutoa mkono wa pole kwa serikali ya Abuja na familia za raia wa nchi hiyo ambao waliuawa katika hujuma hiyo.
-
Abdollahian: Iran itaendelea kuunga mkono muqawama wa Palestina
Jun 06, 2022 23:03Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu katu haitoruhusu kukanyagwa haki za Wairani katika mazungumzo (ya Vienna) au kupuuza haki za wananchi Waislamu wa Palestina na kueleza bayana kuwa, Tehran itaendelea kuunga mkono muqawama wa Wapalestina.
-
Sisitizo la Waziri wa Uchumi na Fedha wa Iran kuhusu kushirikiana nchi za Kiislamu kwa ajili ya kuimarisha uchumi.
Jun 06, 2022 05:38Akizungumza Jumamosi katika kikao cha kila mwaka cha Baraza Kuu la Benki ya Maendeleo ya Kiislamu IDB huKo mjini Cairo Misri, Ehsan Khandouzi, Waziri wa Masuala ya Kiuchumi na Fedha wa Iran, amesisitiza juu ya ulazima wa nchi za Kiislamu kushirikiana kwa ajili ya kuimarisha uthabiti wa kiuchumi wa nchi hizo na kuufanya kuwa na misingi madhubuti zaidi katika kukabiliana na changamoto zilizopo na za baadaye.
-
Iran yamuita balozi wa India kulalamikia kauli za kumvunjia heshima Mtume Muhammad SAW
Jun 05, 2022 23:06Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imemuita balozi wa India mjini Tehran kulalamikia vikali matamshi dhidi ya Mtume Mutukufu wa Uislamu, Muhammad SAW ambayo yalitolewa katika mdahalo wa televisheni huko India na kuibua hasira miongoni mwa Waislamu duniani.
-
Fikra za Imam Khomeini (MA); ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu na kuanza mwamko wa Kiislamu
Jun 04, 2022 04:35Fikra za Imam Khomeini MA za kupambana na ubeberu, mbali na kupelekea kupata ushindi Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, zimepelekea pia kupatikana mwamko wa Kiislamu katika eneo hili zima na duniani kwa ujumla.
-
Baqeri: Wazayuni wanaweza kuwaza ndotoni tu kuishambulia kijeshi Iran
Jun 03, 2022 23:38Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema: Wazayuni wanaweza kuwaza ndotoni tu kuishambulia kijeshi Iran; na wakati wowote ule watakapoota ndoto hiyo hawataweza katu kuamka tena.
-
Tuhuma zisizo na msingi dhidi ya Iran: Saudia haitaki uhusiano mwema wa Iran na nchi za Ghuba ya Uajemi
Jun 03, 2022 02:50Mawaziri wa Nchi wa Masuala ya Kigeni wa nchi za Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi mnamo Juni Mosi kwa mara nyingine walitoa tuhuma nne dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran yajibu matamshi ya Ufaransa, Ujerumani kuhusu meli za mafuta za Ugiriki
Jun 01, 2022 05:28Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametoa taarifa na kukosoa taarifa zinazofanana za Ujerumani na Ufaransa kuhusu meli za mafuta za Ugiriki.
-
Kituo cha Kistratijia cha 313; Nembo ya Uwezo wa Kijeshi wa Iran
May 30, 2022 22:00Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Meja Jenerali Mohammad Baqeri siku ya Jumamosi alikagua kituo kipya cha siri kilicho chini ya ardhi cha ndege zisizo na rubani cha Jeshi la Jamhuri Kiislamu ya Iran. Akiwa hapo alijioenea uwezo mkubwa wa ndege za kivita zisizo na rubani za jeshi hilo zilizoko katika kituo hicho cha siri.
-
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Tajikistan zatiliana saini hati 17 za ushirikiano
May 30, 2022 05:49Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Tajikistan zimetiliana saini hati 17 za ushirikiano katika nyuga tofauti zikiwemo za kisiasa, kiuchumi, kibiashara na kiutalii.