-
Iran: Uzalishaji wa mafuta ghafi umerejea katika kiwango cha kabla ya vikwazo
Apr 01, 2022 22:06Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kiwango cha uzalishaji wa mafuta ghafi ya taifa hili kimeongezeka na kurejea katika kiwango cha kipindi cha kabla ya vikwazo, ilivyowekewa nchi hii na utawala wa Donald Trump baada ya kuiondoa Marekani kwenye mapatano ya nyuklia ya JCPOA mwaka 2018.
-
Mashambulizi dhidi ya askari wa US yameongezeka kwa 400% tangu auawe Soleimani
Apr 01, 2022 22:05Washington imekiri kuwa, tangu Luteni Jenerali Qasem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) auawe kigaidi nchini Iraq, mashambulizi dhidi ya askari wa Marekani yameongezeka kwa asilimia 400.
-
Ershadi: Vikwazo vinatishia haki ya tiba ya wananchi wa Iran
Mar 30, 2022 02:16Balozi na Naibu Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema vikwazo vya upande mmoja vya Marekani ni tishio kubwa kwa haki ya kupata huduma za afya, matibabu na dawa wananchi wa Iran.
-
Marekani yaendeleza msimamo ulio dhidi ya makubaliano ya nyuklia, JCPOA
Mar 27, 2022 23:09Mwakilishi maalumu wa serikali ya Marekani katika masuala ya Iran ameendeleza msimamo wa Washington ulio dhidi ya makubaliano ya nyuklia, JCPOA kwa kudai kwamba, serikali ya sasa haiwezi kutoa hakikisho na dhamana juu ya maamuzi yatakayochukuliwa na serikali ijayo ya Marekani kuhusu makubaliano hayo.
-
Iran na EU zajadili masuala yaliyosalia katika mazungumzo ya Vienna
Mar 27, 2022 07:59Kiongozi wa timu ya Iran katika mazungumzo ya nyuklia ya Vienna, Ali Baqeri Kani amekutana na kufanya mazungumzo hapa mjini Tehran na Enrique Mora, mratibu wa mazungumzo ya Vienna, ambapo wamejadili hatua zilizopigwa na masuala yaliyosalia katika mazungumzo hayo yanayofanyika huko Austria.
-
Iran: Vikosi vamizi vya Marekani viondoke Syria mara moja
Mar 25, 2022 21:53Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema vikosi vya Marekani na waitifaki wake vinapaswa kuondoka Syria haraka iwezekanavyo.
-
Spika wa Lebanon: Iran ndio chimbuko kuu la muqawama katika eneo
Mar 25, 2022 09:53Spika wa Bunge la Lebanon ameitaja Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kama chanzo kikuu cha harakati za muqawama katika eneo la Asia Magharibi, zilizoipa ilhamu kambi ya muqawama kote duniani.
-
Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu mjini Islamabad
Mar 23, 2022 06:16Mkutano wa 48 wa siku mbili wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) ulianza jana Jumanne mjini Islamabad, mji mkuu wa Pakistan.
-
Khatibzadeh: Iran itaendelea kuwa sauti ya ulimwengu wa Kiislamu
Mar 22, 2022 02:01Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu imejitolea kwa dhati kuendelea kupaza sauti ya ulimwengu wa Kiislamu na mataifa yanayodhulumiwa duniani.
-
Kiongozi Muadhamu: Taifa la Iran limefanya machaguo sahihi katika kupambana na Uistikbari
Mar 21, 2022 23:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyid Ali Khamenei amesema kuhusu matukio ya dunia yanayoendelea kujiri katika nchi za Afghanistan, Ukraine na Yemen kwamba: "matukio yote haya yanaonyesha ukweli wa taifa la Iran na machaguo sahihi liliyofanya katika kupambana Uistikbari."