-
Iran yafanyia majaribio makombora mapya ya cruise
Jun 18, 2020 14:01Jeshi la Baharini la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limefanyia majaribio kwa mafanikio makombora yake mapya ya cruise katika luteka ya kijeshi iliyofanyika kaskazini mwa Bahari ya Hindi na katika Bahari ya Oman.
-
Iran: Tutaendelea kuliunga mkono taifa la Syria, muqawama
Jun 18, 2020 12:33Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu itaendelea kuliunga mkono na kusimama na taifa la Syria pamoja na kambi ya muqawama katika eneo.
-
Iran: Badala ya kuwa na wasi wasi usio na msingi, Troika ya Ulaya itekeleze ahadi zake JCPOA
Jun 17, 2020 22:58Mkuu wa Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa taarifa ya Troika ya Ulaya, yaani Ujerumani, Uingereza na Ufaransa, kuhusu mapatano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) na shughuli za nyuklia za Iran zenye malengo ya amani.
-
Iran: Bodi ya Magavana ya IAEA isithubutu kuchukua hatua isiyo na maana
Jun 15, 2020 10:30Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu itatoa jibu mwafaka kwa hatua yoyote hasi na isiyo na maana itakayochukuliwa na Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa ya Nishati ya Atomiki (IAEA) dhidi ya taifa hili, kwa kutegemea madai yasiyo na msingi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Zarif asema uhusiano wa Iran na Uturuki katika nyuga tofauti ni wa karibu sana
Jun 15, 2020 03:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu na Uturuki zina uhusiano mzuri wa na karibu sana katika nyuga mbali mbali.
-
Palestina yataka kikao cha Baraza la Usalama kijadili Israel kughusubu Ukingo wa Magharibi
Jun 14, 2020 03:38Rais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ametoa wito wa kikao kijacho cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kifanyike katika ngazi ya juu itakayojumuisha mawaziri wa mambo ya nje badala ya wawakilishi wakati wa kujadiliwa mpango tata wa Israel wa kuteka na kughusubu maeneo zaidi ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Shamkhani: Kuvunjwa 'masanamu ya kibaguzi' kumewatia kiwewe Wazayuni
Jun 13, 2020 08:06Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kitendo cha kuvunjwa nembo na masanamu yanayoashiria ubaguzi wa rangi katika nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani kimeutia kiwewe na wahka mkubwa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
China yapinga kurefushwa vikwazo vya silaha dhidi ya Iran
Jun 12, 2020 23:41Kwa mara nyingine tena China imepinga vikali njama za Marekani za kutaka kurefushwa muda wa vikwazo vya silaha dhidi ya Iran. Muda wa vikwazo hivyo unafikia tamati Oktoba mwaka huu wa 2020, kwa mujibu wa Azimio Nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Matokeo mabaya ya vitendo viovu vya Marekani dhidi ya Iran; kuendelea kuvunjwa sheria duniani
Jun 12, 2020 05:47Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Marekani haina haki ya kuutumia vibaya Umoja wa Mataifa na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA kuiharibia jina Iran.
-
Zarif: Marekani mara hii inatumia mabavu dhidi ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai
Jun 12, 2020 03:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria hatua ya Marekani kuwawekea vikwazo maafisa kadhaa wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) na kusema, hivi sasa ICC inahujumiwa na genge la wahalifu wambao wanajiarifisha kuwa ni wanadiplomasia."