-
Jeshi la Iran lasema haliwezi kupigishwa magoti na maadui
Apr 23, 2018 03:31Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katu Iran haiwezi kupigishwa magoti na kukubali matakwa ya maadui wa taifa hili wakiongozwa na Marekani na waitifaki wake.
-
Macron: Ufaransa haina mpango mwingine mbadala wa makubaliano ya JCPOA
Apr 22, 2018 23:32Rais wa Ufaransa ameashiria kuwa Paris haina mpango mwingine mbadala wa makubaliano ya JCPOA na kuitaka Marekani isalie katika makubaliano hayo ya pamoja na Iran.
-
Iran na Benin kuimarisha uhusiano wao katika uga wa viwanda
Apr 22, 2018 20:55Balozi wa Benin hapa mjini Tehran, Naim Akibo amesema akthari ya nchi za Afrika hazijadiriki uwezo mkubwa wa Iran katika nyuga za viwanda, kilimo na uchumi ambao zingeutumia katika kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa pande mbili.
-
Iran: Ripoti ya haki za binadamu ya Marekani ni ya kiuadui na kisiasa na haikubaliki
Apr 22, 2018 03:32Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa jibu kwa ripoti ya kila mwaka inayotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani kuhusu haki za binadamu kwa kueleza kwamba ripoti hiyo ni ya kiuadui na kisiasa na haikubaliki.
-
Iran: Kama mapatano ya JCPOA yatavunjika, tutaanza kutekeleza miradi yetu ya nyuklia kwa kasi kubwa
Apr 21, 2018 23:40Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuhusu uwezekano wa Marekani kujitoa katika mapatano ya nyuklia yanayojulikana kwa jina maarufu la JCPOA kwamba, Tehran ina machaguo kadhaa likiwemo la kuanzisha utekelezaji wa miradi yake ya nyuklia kwa kasi kubwa zaidi.
-
Jaberi Ansari afanya mazungumzo na mjumbe wa UN katika masuala ya Syria
Apr 21, 2018 09:38Mjumbe maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Syria leo amekutana na kufanya mazungumzo hapa mjini Tehran na Hossein Jaberi Ansar msaidizi mkuu wa Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran katika masuala ya siasa.
-
Russia: Mradi wa makombora wa Iran hauna uhusiano wowote na JCPOA
Apr 21, 2018 02:57Balozi wa Russia mjini Tehran amesisitiza kuwa, mradi wa makombora wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na siasa za Tehran kuhusiana na eneo hili hazina uhusiano wowote na maafikiano ya nyuklia yanayojulikana kwa jina la JCPOA.
-
Zarif: Marekani itajuta kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Iran
Apr 20, 2018 02:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Javad Zarif amesema Tehran ina hatua kadhaa ambazo inaweza kuchukua ambazo zitaifanya Marekani ijute kujiondoa katika mapatano ya nyuklia yajulikanayo kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA.
-
Iran yaonyesha uwezo wake mkubwa wa kijeshi katika Siku ya Taifa ya Jeshi
Apr 18, 2018 03:21Rais Hassan Rouhani amesema uwezo mkubwa wa kijeshi na kiulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kwa ajili ya kujihami na wala sio kwa sababu ya kuivamia nchi yeyote au kudhuru maslahi yao.
-
Rouhani: Iran na Uturuki zitaendelea kushirikiana ili kuzima taharuki Syria
Apr 18, 2018 03:00Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mashambulizi ya hivi karibuni ya kijeshi yaliyofanywa na Marekani, Uingereza na Ufaransa dhidi ya Syria yameacha mfano wenye sura ya kutisha kwenye uhusiano wa kimataifa, na kusisitiza kwamba Iran na Uturuki zitaendelea kuwa na ushirikiano wa karibu kwa lengo la kuzuia kushtadi taharuki katika nchi hiyo ya Kiarabu.