-
Iran: Tutaendelea daima kutetea haki za taifa linalodhulumiwa la Palestina
Mar 04, 2018 13:21Msaidizi maalumu wa Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) anayehusika na masuala ya kimataifa amesema katika mazungumzo yake na balozi wa Palestina hapa mjini Tehran kwamba Jahuri ya Kiislamu ya Iran daima itaendelea kupigania haki zilizoporwa za taifa la Palestina.
-
Ufaransa yasisitiza kuheshimu makubaliano ya nyuklia ya JCPOA
Mar 04, 2018 13:10Viongozi wa Ufaransa wamesisitiza tena misimamo yao juu ya kuyalinda na kuyaheshimu makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA).
-
Iran ina ushahidi kuhusu uhusiano wa Marekani na Daesh (ISIS)
Mar 04, 2018 04:30Msaidizi Maalumu wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kimataifa amesema vyombo vya usalama vya Iran vina ithibati kuhusu uhusiano kati ya Marekani na kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS).
-
Iran: Hatufanyi mazungumzo na EU kuhusu kuimarika ushawishi wetu M/Kati
Mar 04, 2018 00:02Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekadhibisha ripoti zilizodai kuwa Tehran na nchi kadhaa za Umoja wa Ulaya EU zimeanza kufanya mazungumzo kuhusu nafasi ya taifa hili katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Jumapili, Machi 4, 2018
Mar 03, 2018 23:06Leo ni Jumapili tarehe 15 Jamadith-Thani mwaka 1439 Hijiria, mwafaka na tarehe 4 Machi, mwaka 2018 Miladia.
-
Israel: Tumepoteza uwezo wetu mkubwa mbele ya harakati ya Hizbullah na Hamas
Mar 03, 2018 01:38Kamanda wa vikosi vya ardhini vya utawala haramu wa lsrael amekiri kwamba, jeshi la utawala huo limepoteza uwezo wake mkubwa mkabala wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon na Harakati ya muqawama wa Palestina HAMAS.
-
Boroujerdi: Iran haina mahusiano yoyote ya kiuchumi, kimichezo na kisiasa na Israel
Mar 02, 2018 10:26Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Kigeni ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran), Alaeddin Boroujerdi sambamba na kubainisha kwamba michezo ni sehemu ndogo ya mahusiano yaliyokatwa mapema kati ya Iran na Israel, amesema kuwa mfumo wa Iran ya Kiislamu kamwe hauna mahusiano ya kiuchumi na kisiasa na utawala huo bandia.
-
Qassemi: Ripoti ya Antonio Guterres kuhusu hali ya haki za binadamu Iran haina itibari
Mar 02, 2018 00:30Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, ripoti ya Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Iran haina itibari wala thamani kutokana na kutoakisi ukweli.
-
Iran yazilaumu vikali nchi zinazomiliki silaha za nyuklia
Mar 01, 2018 12:00Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezilaumu vikali nchi zinazomiliki silaha za nyuklia kwa kutoheshimu ahadi zao kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Mkataba wa Kuzuia Uzalishaji, Uenezaji na Utumiaji wa Silaha za Nyuklia na kusema kuwa nchi hizo ndizo zinazokwamisha ufanikishaji wa vipengee vya mkabata huo.
-
Iran: Tutajiondoa kwenye makubaliano ya nyuklia iwapo hayatakuwa na maslahi kwetu
Feb 28, 2018 04:35Msemaji wa serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Tehran itajiondoa mara moja kwenye makubaliano ya nyuklia iwapo itahisi mapatano hayo hayana maslahi kwa taifa hili.