-
HAMAS: Israel imekiuka vipengele vyote vya usitishaji vita, makubaliano yako hatarini kuvunjika
Dec 17, 2025 03:09Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina HAMAS ameushutumu utawala wa kizayuni wa Israel kwa ukiukaji mkubwa na uliopangwa wa makubaliano ya kusitisha vita, akionya kwamba kuendelea kwa mwelekeo huo kunayaweka makubaliano hayo katika hatari ya kuvunjika kikamilifu.
-
ICC yatupilia mbali rufaa ya Israel ya kuomba waranti wa kumkamata Netanyahu ubatilishwe
Dec 15, 2025 23:57Kitengo cha rufani cha Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC kimetupilia mbali hoja za utawala wa kizayuni wa Israel za kupinga uhalali wa uchunguzi wa mahakama hiyo kuhusu jinai zilizofanywa Ukanda wa Ghaza kufuatia vita vya kinyama na vya mauaji ya kimbari ambavyo utawala huo haramu ulivianzisha Oktoba 7, 2023 dhidi ya Wapalestina wa ukanda huo uliowekewa mzingiro.
-
Yemen yaonya kuhusu kushtadi jinai za Israel Gaza, Ukingo wa Magharibi
Dec 15, 2025 07:29Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen imetahadharisha dhidi ya kuongezeka kwa ukatili unaofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina huko Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu, ikiukosoa utawala huo pandikizi kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano na kuzidisha mashambulizi.
-
Azimio jipya la Baraza Kuu la UN; Msimamo wa kimataifa dhidi ya utawala wa Kizayuni
Dec 13, 2025 22:36Sambamba na Israel kukiuka usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio jipya linaloitaka Tel Aviv kutekeleza uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kuhusu eneo hilo la Palestina.
-
Albanese: Israel na waungaji mkono wake wakuu inawapasa wagharamie ujenzi mpya wa Ghaza
Dec 13, 2025 08:06Francesca Albanese, Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu amesema, Israel na Marekani pamoja na nchi zingine ambazo zilikuwa wasambazaji wakuu wa silaha kwa utawala huo, zinapaswa kugharimia ujenzi mpya wa eneo la Ukanda wa Ghaza.
-
Kuongezeka idadi ya nchi zilizosusia Mashindano ya Eurovision kulalamikia kushirikishwa utawala wa Kizayuni
Dec 13, 2025 05:54Idadi ya nchi zilizosusia mashindano ya Eurovision zikipinga kushirikishwa utawala wa Kizayuni katika mashindano hayo, imeongezeka.
-
Baraza Kuu la UN lapasisha azimio la kuitaka Israel iondoe vizuizi vya msaada Gaza
Dec 12, 2025 23:19Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepasisha rasimu ya azimio linaloitaka Israel kuruhusu kutolewa kwa huduma za kibinadamu pasi na vikwazo na vizingiti katika Ukanda wa Gaza.
-
Israel yakiri: Tulisababisha uharibifu mdogo kwa Iran kuliko ilivyodhaniwa hapo awali
Dec 12, 2025 23:03Israel imekiri kuwa ilisababisha uharibifu wa kiwango kidogo kwa Iran wakati wa vita vya siku 12 mwezi Juni mwaka huu kuliko ilivyofikiriwa awali.
-
Upinzani mkubwa wa UN dhidi ya kubadilishwa mipaka ya Gaza
Dec 12, 2025 08:55Umoja wa Mataifa umetangaza upinzani wake mkubwa dhidi ya kufanyika mabadiliko ya aina yoyote ya mipaka ya Gaza na utawala wa Israel.
-
Iran yalaani mwenendo wa madola makubwa wa kuitunukia Israel 'haki maalumu' ya kufanyia uchokozi
Dec 12, 2025 07:33Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, sera za mataifa makubwa katika Asia Magharibi zimetengeneza "haki maalumu kwa ajili ya utawala wa Kizayuni," hali ambayo imeiwezesha Israel kufanya uchokozi wa kijeshi katika eneo zima, ikiwa ni pamoja na dhidi ya Iran, bila kukabiliwa na mjibizo wa maana kimataifa kwa uchokozi wake huo.