-
Iran yalaani mashambulizi ya kinyama ya Israel dhidi ya Syria
Mar 09, 2023 23:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani wimbi la mashambulizi ya kikatili ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Syria, wakati huu ambapo taifa hilo linakabiliwa na matatizo chungu nzima kutoka na maafa makubwa ya matetemeko ya ardhi.
-
Afrika Kusini katika mchakato wa kupunguza kiwango cha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel
Mar 09, 2023 22:54Bunge la Afrika Kusini limetangaza kupitisha sheria ya kupunguza kiwango cha uhusiano wake na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kusisitiza kwamba utawala huo unaozikoloni ardhi za Palestina ni utawala wa kibaguzi au apathaidi ambao unawadhulumu na kuwabagua Wapalestina.
-
'Pango la Simba' kulipiza kisasi cha mauaji ya Wapalestina Jenin
Mar 08, 2023 06:23Kundi la Muqawama wa Kiislamu la Arin al Usud (Pango la Simba) limesema litalipiza kisasi cha mauaji ya kikatili ya Wapalestina katika mji wa Jenin katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Afrika Kusini kupunguza kiwango cha uhusiano wake na utawala wa Kizayuni wa Israel
Mar 08, 2023 03:09Bunge la Afrika Kusini jana Jumanne lilipiga kura ya kuunga mkono kushushwa hadhi ya ubalozi wa nchi hiyo huko Israel kutokana na kuendelea unyanyasaji na mauaji ya utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Mash'al: Kuanzisha uhusiano na Israel umeisababishia Palestina dhiki
Mar 05, 2023 07:28Kiongozi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) nje ya nchi ameyakosoa baadhi ya madola ya Kiarabu kwa kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel na kusisitiza kuwa, ushirikiano na utawala huo wa Kizayuni haujakuwa na matokeo mengine ghairi ya kuwasababishia Wapalestina dhiki na matatizo.
-
"Mkutano wa Aqaba unaipa Israel kibali cha kushadidisha jinai dhidi ya Wapalestina"
Feb 27, 2023 06:13Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameashiria mkutano eti wa kiusalama ulioandaliwa na Marekani huko Jordan na kusisitiza kuwa, kikao hicho cha Aqaba kinalenga kuupa utawala wa Kizayuni wa Israel ridhaa ya kushadidisha jinai zake dhidi ya Wapalestina.
-
Iran: Kusambaratika Israel hakuepukiki licha ya uungaji mkono wa US
Feb 23, 2023 23:37Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema utawala haramu wa Israel upo katika ncha ya kusambaratika na kutokomea, licha ya uungaji mkono.
-
Oman yaruhusu ndege za Israel zitumie anga yake
Feb 23, 2023 23:36Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel amedai kuwa, Oman imeidhinisha ndege za utawala huo haramu kuruka katika anga ya nchi hiyo ya Ghuba ya Uajemi.
-
Baraza la Usalama lalaani ujenzi wa vitongoji haramu Palestina inayokaliwa kwa mabavu
Feb 21, 2023 03:51Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepasisha rasimu ya azimio linalolaani uamuzi wa serikali ya Israel yenye misimamo ya kufurutu ada ya Benjamin Netanyahu wa kuidhinisha ujenzi wa vitongoji vipya tisa katika ardhi za Wapalestina za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Nchi za Amerika ya Latini zalaani ujenzi wa vitongoji haramu
Feb 18, 2023 06:23Kundi la nchi za Amerika ya Latini limelaani na kukosoa vikali uamuzi wa serikali ya Israel yenye misimamo ya kufurutu ada ya Benjamin Netanyahu wa kuidhinisha ujenzi wa vitongoji vipya tisa katika ardhi za Wapalestina za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.