-
Hizbullah: Zama za Israel kufanya mashambulizi bila majibu zimepita
Feb 12, 2018 04:21Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, zile zama za utawala wa Kizayuni wa Israel kufanya mashambulizi na kuachiwa vivi hivi bila ya majibu zimeisha na kuanzia sasa shambulio lolote la Wazayuni litajibiwa vikali.
-
Israel yabomoa shule za EU huko Palestina inyaokaliwa kwa mabavu
Feb 09, 2018 11:00Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuwa, Wapalestina na Mabedui wanaoishi katika kitongoji cha Area C katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan huko Palestina wapo katika hatari ya kufurushwa kwenye makazi yao na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Rais wa Lebanon asema jeshi la nchi hiyo liko tayari kuikabili Israel
Feb 09, 2018 10:39Rais wa Lebanon ameliagiza jeshi la nchi hiyo kuwa macho dhidi ya njama zozote za utawala haramu wa Israel za kujaribu kudhalilisha uhuru wa kujitawala nchi hiyo.
-
Mwanaharakati wa kike aliyekosoa mahusiano ya Saudia na Israel aendelea kushikiliwa Riyadh
Feb 08, 2018 10:54Mwanaharakati wa kike ambaye alikosoa kitendo cha kuanzishwa mahusiano kati ya nchi za Kiarabu zikiongozwa na Saudia, na utawala haramu wa Israel, anaendelea kushikiliwa katika korokoro za kutisha za utawala wa Aal Saud.
-
Saudia yafungua rasmi anga yake kwa ajili ya ndege zinazokwenda Israel
Feb 08, 2018 00:28Kwa mara ya kwanza kabisa katika historia, Saudi Arabia imefungua anga yake kwa ajili ya ndege zinazoelekea katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni tangu mwaka 1948 ambazo zimebadilishwa jina na kuitwa Israel.
-
Jeshi la Israel lamuua shahidi kijana wa Palestina
Feb 07, 2018 04:41Wanajeshi katili wa utawala haramu wa Israel wamemuua shahidi Mpalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, kwa tuhuma kuwa alitaka kumdunga kisu askari wa Kizayuni.
-
Jeshi la Syria lajibu mapigo, latungua makombora ya Israel
Feb 07, 2018 04:06Jeshi la Syria limetoa jibu kali kwa uvamizi mpya wa Israel, baada ya utawala huo wa Kizayuni kuanzisha mashambulizi ya makombora viungani mwa mji mkuu wa nchi hiyo, Damascus.
-
Viongozi wa Lebanon wasema Israel ni tishio kwa usalama mpakani
Feb 06, 2018 10:47Viongozi watatu wa ngazi za juu nchini Lebanon wamesema utawala haramu wa Israel ni tishio kwa uthabiti wa eneo la mpakani.
-
Mwanamfalme wa Bahrain atembelea Israel, atazamiwa kuhudhuria bunge
Feb 05, 2018 13:07Waziri wa Mawasiliano wa utawala wa Kizayuni wa Israel Ayoub Kara amethibitisha kuwa amekutana na mwanamfalme wa Bahrain Mubarak Aal Khalifa mjini Tel Aviv.
-
Israel yaanza kuwapa wahajiri wa Afrika ilani ya kutimuliwa
Feb 05, 2018 01:08Utawala wa Kizayuni wa Israel umeanza kuwapa ilani ya kutimuliwa maelfu ya wahajiri wa Kiafrika walioingia katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo haramu.