Israel yaanza kuwapa wahajiri wa Afrika ilani ya kutimuliwa
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i39923-israel_yaanza_kuwapa_wahajiri_wa_afrika_ilani_ya_kutimuliwa
Utawala wa Kizayuni wa Israel umeanza kuwapa ilani ya kutimuliwa maelfu ya wahajiri wa Kiafrika walioingia katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo haramu.
(last modified 2023-11-27T12:14:11+00:00 )
Feb 05, 2018 04:38 UTC
  • Israel yaanza kuwapa wahajiri wa Afrika ilani ya kutimuliwa

Utawala wa Kizayuni wa Israel umeanza kuwapa ilani ya kutimuliwa maelfu ya wahajiri wa Kiafrika walioingia katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala huo haramu.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AP, wahajiri hao walianza kupewa barua hizo za notisi jana Jumapili na kupewa siku 60 wawe wameondoka, na ambao hawataondoka kufikia Aprili Mosi, watakamatwa na kuzuiliwa kwa muda usiojulikana.

Mapema mwezi huu, utawala huo batili ulitangaza kuanza kutekeleza mpango wa kuwarejesha nchini kwao kwa nguvu makumi ya maelfu ya Waafrika

Mpango huu ambao uliidhinishwa na baraza la mawaziri la Israel mwezi Novemba mwaka jana uliibua malalamiko kutoka taasisi nyingi za kimataifa likiwemo Shirika la Kuwahudumia Wakimbizi la Umoja UNHCR.

Maafisa katili wa Israel wakiwashambulia wahajiri wa Kiafrika

Wengi wa wahajiri hao ni kutoka Sudan na Eritrea na wamekuwa wakiingia katika ardhi hizo za Palestina kupitia mpaka wa jangwani na Misri.

Israel ilidai kuwa imeafikiana na Rwanda na Uganda juu ya kuwakabidhi wahajiri hao kwa nchi hizo , licha ya viongozi wa nchi hizo za mashariki mwa Afrika kukanusha habari hizo.