-
Erdogan: Netanyahu ni chinjachinja wa Gaza anayetaka kurefusha maisha yake ya kisiasa
Nov 30, 2023 22:58Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amemtaja Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, kuwa ni "mchinjaji wa Gaza," akisisitiza kwamba anarikodi jina lake katika historia kwa sifa hiyo kwa sababu "amefanya moja ya ukatili mkubwa zaidi wa karne hii."
-
Wito wa Umoja wa Mataifa kuhusu usitishaji vita wa kudumu huko Gaza na onyo la kuenea mapigano
Nov 30, 2023 06:13Siku ya Jumanne, ikiwa ni siku ya tano ya usitishaji vita wa muda huko Gaza, Umoja wa Mataifa ulifanya vikao viwili, kimoja katika Baraza Kuu kuhadili vita kati ya Israel na Hamas na kingine katika Baraza la Usalama kuhusu hali ya Mashariki ya Kati na Syria, ambapo vikao vyote viwili vilizungumzia kuenea mapigano katika eneo na kusisitiza juu ya udhrura wa kutekelezwa usitishaji vita wa kudumu.
-
Israel yaendelea kumwaga damu za watoto wadogo Jenin
Nov 30, 2023 00:24Watoto wawili wa Kipalestina wameuawa shahidi kwa kupigwa risasi na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika mji wa Jenin, kaskazini ya eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Iran yazionya Marekani na Israel juu ya 'matokeo hasi makali' endapo jinai za kivita zitaendelea Gaza
Nov 28, 2023 09:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian amezionya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwamba zitakabiliwa na "matokeo hasi makali" iwapo zitashindwa kukomesha kikamilifu uhalifu wa kivita katika Ukanda wa Gaza uliofanywa wakati wa vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya eneo Palestina lililowekewa mzingiro.
-
Israel yaua shahidi Wapalestina 4 Jenin, Ukingo wa Magharibi
Nov 25, 2023 23:47Vijana wanne wa Kipalestina wameuawa shahidi kwa kupigwa risasi na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika mji wa Jenin, kaskazini ya eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Uhispania na Ubelgiji zatangaza kuwa tayari kuitambua rasmi nchi ya Palestina
Nov 25, 2023 08:17Hatua ya Uhispania na Ubelgiji ya kutangaza kuwa tayari kuitambua rasmi nchi huru ya Palestina ni tukio muhimu kushuhudiwa barani Ulaya kuhusu kadhia ya Palestina. Hatua hii imeukasirisha sana utawala wa Kizayuni.
-
Abu Ubaida atangaza baadhi ya hasara za Israel katika Kimbunga cha al Aqsa
Nov 25, 2023 01:05Msemaji wa Brigedi za Izzuddin al-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS), ametangaza kwamba zana na ala 335 za jeshi la Israel zimeharibiwa kabisa tangu kuanza mashambulizi ya utawala huo haramu dhidi ya watu wa Gaza na kusisitiza kuwa, utawala vamizi umelazimika kukubali suluhu na kusitisha mapigano.
-
Afrika Kusini yataka Israel itambulishwe kama "utawala wa kibaguzi"
Nov 25, 2023 01:04Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini ametangaza kwamba nchi hiyo inaendeleza juhudi katika mashirika na jumuiya za kimataifa za kuutambulisha utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa ni "utawala wa kibaguzi".
-
Amir-Abdollahian: Uungaji mkono wa Marekani kwa Israel ulisababisha kuendelea kwa vita Gaza
Nov 24, 2023 08:32Waziri wa Mashauriano ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kama si msaada na himaya ya Marekani kwa utawala ghasibu wa Israel, utawala huo bandia haungeweza kuendeleza vita na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS).
-
70% ya vijana Marekani wanapinga Biden kuikingia kifua Israel
Nov 23, 2023 04:03Uchunguzi mpya wa maoni uliofanywa nchini Marekani unaonyesha kuwa, aghalabu ya vijana nchini humo hawaungi mkono msimamo wa Rais Joe Biden kwa mashambulizi ya mabomu, jinai za kivita na uporoaji wa ardhi unaofanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya Palestina.