-
UN: Ebola inaua mtu mmoja kila baada ya nusu saa huko Congo DR
Aug 16, 2026 03:17Tom Fletcher, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Masuala ya Kibinadamu, ametangaza kwamba mlipuko wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo sasa unaua mtu mmoja kila baada ya nusu saa, akitoa wito kwa jamii ya kimataifa kuchukua hatua za haraka kupambana na mlipuko huo.
-
Kongo: Mkurugenzi Mkuu wa WHO atahadharisha kuhusu mlipuko wa Ebola
Aug 13, 2026 03:39Baada ya kurejea kutoka ziarani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ametahadharisha kuhusu mlipuko wa Ebola.
-
DRC yajipanga kwa sensa ya kwanza ya kitaifa baada ya miaka 42
Aug 10, 2026 03:12Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) inajiandaa kufanya sensa yake ya kwanza ya kitaifa baada ya zaidi ya miongo minne, kazi kubwa inayolenga kuwapatia hadhi rasmi mamilioni ya raia ambao wameishi bila vitambulisho vya kitaifa vilivyotolewa na serikali.
-
UN: Watoto zaidi ya 300 wamefariki dunia kwa Ebola tangu kuanza mlipuko huo huko Kongo
Aug 08, 2026 12:55Watoto zaidi ya 300 wamefariki dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola tangu mlipuko huo uliopoikumba Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Idadi hii ni kwa mujibu wa takwimu zilizotangazwa jana Naibu Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Farhan Haq.
-
Mlipuko wa Ebola Kongo wapindukia maambukizi 4,000
Aug 08, 2026 02:42Idadi ya kesi za Ebola zilizothibitishwa hadi kufikia jana Ijumaa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zilikuwa zimepindukia 4,000 huku maeneo ya afya yaliyoathirika yakiongezeka.
-
Kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya Ebola DRC huku maambukizi yakienea
Aug 06, 2026 03:49Kituo kikubwa zaidi cha matibabu ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kimefunguliwa wiki hii na wadau wa Umoja wa Mataifa ikiwa ni hatua inayolenga kuimarisha mwitikio dhidi ya mlipuko wa sasa wa virusi vya Ebola aina ya Bundibugyo unaoendelea kuenea kwa kasi katika jimbo la Ituri, mashariki mwa taifa hilo.
-
Africa CDC yatoa tahadhari kufuatia mlipuko wa Ebola Kongo kushindwa kudhibitiwa
Aug 05, 2026 12:08Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa barani Afrika ( AFRICA CDC) kimetahadharisha kuwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo unazidi kuwa nje ya udhibiti, huku vifo zaidi ya 1,700 vikirekodiwa ndani ya wiki 14 pekee. Hii ni katika hali ambayo juhudi za kuwafuatilia watu waliotangamana na wagonjwa zimeshindwa kudhibiti msambao wa virusi hivyo.
-
Utafiti: Mlipuko wa Ebola Kongo ulianza miezi kadhaa kabla ya kugunduliwa
Aug 01, 2026 11:24Utafiti: Mlipuko wa Ebola Kongo ulianza miezi kadhaa kabla ya kugunduliwa
-
Upinzani DRC wakasirika baada ya Mahakama kumfungulia njia rais Tshisekedi kugombea muhula wa tatu
Jul 30, 2026 10:19Wanasiasa wa upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC, ambao ni wanachama wa muungano wa upinzani uliopewa jina la utani "C64", wamepinga vikali uamuzi wa Mahakama ya Katiba kuhusu sheria ya kura ya maoni, ambayo inaweza kumfungulia njia Rais wa nchi hiyo Felix Tshisekedi kugombea urais kwa muhula wa tatu baada ya kura hiyo ya maoni.
-
Maambukizi ya Ebola DRC yakaribia 3,000 huku vifo vikifikia 1,269
Jul 25, 2026 03:03Maambukizi ya virusi vya Ebola yameongezeka kwa kasi na kufikia karibu kesi 3,000 zilizothibitishwa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), huku vifo vikizidi 1,260. Hali hii inajiri baada ya mamlaka za afya kuoanisha kanzidata za mikoa na zile za kitaifa, sambamba na kuripotiwa kwa makumi ya kesi mpya katika kitovu cha mlipuko wa virusi hivyo.