-
DRC, M23 zasaini makubaliano ya kubuni utaratibu wa usitishaji mapigano
Oct 15, 2025 11:42Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kundi la waasi la M23 wametia saini makubaliano mjini Doha ya kuanzisha utaratibu wa ufuatiliaji na uhakiki wa usitishaji mapigano, chini ya upatanishi wa Qatar.
-
ICRC: Mgogoro wa afya Kongo DR unazidi kuwa mbaya
Oct 09, 2025 03:11Mfumo wa huduma za afya katika eneo linalokumbwa na migogoro mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umezorota kwa kiasi kikubwa, huku vituo vingi vya matibabu vikiwa na uhaba mkubwa wa dawa na wafanyakazi, Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) imeonya katika taarifa yake ya jana Jumatano.
-
Mripuko wa Ebola: Kesi kumi na moja zathibitishwa nchini Kongo
Sep 26, 2025 02:29Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inakabiliana na mripuko mpya wa ugonjwa wa Ebola, huku maafisa wa afya wakithibitisha kesi kumi na moja za ziada katika Ukanda wa Afya wa Bulape katika Mkoa wa Kasai.
-
Waasi wa M23 wauteka tena mji wa Shoa katika jimbo la Kivu kaskazini
Sep 08, 2025 07:32Waasi wa kundi la M23 jana waliuteka tena mji wa Shoa katika jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya mapigano na wanajeshi wanaoiunga mkono serikali ya Kinshasa.
-
DRC yatangaza mripuko wa 16 wa Ebola; WHO yatoa indhari
Sep 05, 2025 10:38Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetangaza mripuko mpya wa Ebola katika jimbo la kati la Kasai, ambalo ni la 16 nchini humo tangu 1976, huku Shirika la Afya Duniani (WHO) likitahadharisha kuwa huenda maambukizi ya maradhi hayo yakaongezeka.
-
Kinshasa na M23 waanza tena mazungumzo Qatar katika juhudi za kutekeleza makubaliano ya kusitisha vita
Aug 27, 2025 10:49Duru mpya ya mazungumzo kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na waasi wa M23 inaendelea katika mji mkuu wa Qatar, Doha. Pande hizo mbili zinatazamia kufikia makubaliano juu ya namna ya kutekeleza mapatano waliyosaini mwezi uliopita kwa upatanishi wa Qatar.
-
Mwendesha mashtaka wa DRC ataka Kabila ahukumiwe kifo
Aug 23, 2025 06:15Mwendesha mashtaka wa kijeshi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametoa mwito wa kutolewa hukumu ya kifo dhidi ya rais wa zamani wa nchi hiyo, Joseph Kabila ambaye mashitaka dhidi yake yanaendelea bila ya yeye kuwepo mahakamani.
-
Amnesty International: Haki za binadamu zimekiukwa mashariki mwa Kongo
Aug 22, 2025 02:12Shirika la Msamaha Duniani, Amnesty International, limezituhumu pande zinazozozana mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa kufanya ukiukwaji wa kutisha wa haki za binadamu ikiwa ni pamoja na vitendo vya kubaka kwa umati, mauaji ya kiholela na utekaji nyara.
-
HRW: Waasi wa M23 wameuwa raia zaidi ya 140 mashariki mwa Kongo
Aug 20, 2025 11:58Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch (HRW) limeeleza hii leo kuwa waasi wa kundi la M23 limeuwa raia zaidi ya 140 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Matumaini ya kupatikana suluhisho la kisiasa baina ya serikali ya Kongo DR na M23 yaongezeka
Aug 19, 2025 03:04Matarajio ya kufikiwa suluhisho la amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yameongeka baada ya miongo kadhaa ya vita vya kikatili mashariki mwa nchi hiyo.