Jan 16, 2023 10:47
Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani vikali shambulio lililotokea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC wakati wa ibada ya Jumapili katika kanisa moja huko Kasindi, jimboni Kivu Kaskazini na kusisitiza haja ya kuwawajibisha wahusika wa shambulio hilo.