Nov 04, 2022 11:25
Wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wenye hasira wamechoma moto bendera ya Umoja wa Ulaya katika mji wa Bukavu mashariki mwa nchi hiyo, huku mamia ya wakiandamana dhidi ya waasi wa M23. Wananchi hao wameeleza kutoridhishwa kwao na uingiliaji wa mataifa makubwa kama vile Marekani, Uingereza na Ufaransa katika masuala ya ndani ya nchi yao.