-
Waziri wa zamani wa DRC ataka Rwanda ivamiwe na kugeuzwa mkoa ili mashariki mwa DRC kuwe salama + Sauti
Dec 25, 2019 07:14Waziri Mkuu wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Adolphe Muzito amesema kuwa, njia pekee ya kumaliza uasi mashariki mwa nchi hiyo ni kuivamia nchi jirani ya Rwanda na kuigeuza kuwa mkoa wa DRC. Mossi Mwasi na maelezo zaidi.
-
Mashinikizo ya wananchi yailazimisha serikali DRC kufuta sherehe za kukabidhiwa madaraka Tshisekedi + Sauti
Dec 23, 2019 06:29Serikali ya jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imelazimika kufutilia mbali sherehe za kupokezana madaraka kwa njia ya amani baina ya rais mstaafu wa nchi hiyo Joseph Kabila na rais wa hivi sasa Felix Tshisekedi. Hii in baada ya wananchi na asasi za kiraia kulalamikia gharama kubwa za hafla hizo zilizotazamiwa kufanyika tarehe 24 Januari mwakani. Mwandishi wetu Mossi mwazi na maelezo zaidi.
-
Jeshi la DRC laikabidhi Rwanda waasi 71 wa Kihutu
Dec 22, 2019 10:37Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limeikabidhi Rwanda mamia ya Wanyarwanda wanaohusishwa na kundi moja la waasi la Rwanda linaloendesha harakati zake mashariki mwa DRC.
-
Machafuko yawafanya Wakongomani karibu laki 7 kuhama makazi yao
Dec 19, 2019 21:38Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka limesema karibu watu laki saba katika maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamelazimika kuhama makazi yao na kuwa wakimbizi wa ndani kutokana na kushtadi ghasia na mapigano.
-
Watu 22 wauawa katika shambulio la kigaidi la waasi wa ADF mashariki wa DRC
Dec 16, 2019 23:39Watu wasiopungua 22 wameuawa katika mji wa Beni wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia mashambulio ya kudi la waasi la ADF la Uganda.
-
Watu elfu 5 wafariki dunia kwa Typhoid Kongo DR
Dec 06, 2019 04:01Shirika la Afya Duniani WHO limetangaza habari ya kufariki dunia watu elfu tano kutokana na homa ya matumbo (Typhoid) huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Jeshi la Kongo DR lasema limeua makumi ya wanamgambo wa ADF
Dec 04, 2019 03:50Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limetangaza habari ya kuwauwa wanamgambo zaidi ya 80 wa ADF Nalu mjini Beni, mashariki mwa nchi, katika operesheni dhidi ya makundi ya wapiganaji waliojizatiti kwa silaha.
-
Wasiwasi wa UNCHR kuhusu kuenea machafuko mashariki mwa DRC
Nov 30, 2019 04:14Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limesema lina wasiwasi mkubwa kuhusu maisha ya raia wakiwemo wakimbizi wa ndani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC ambako machafuko yanazidi kushika kasi.
-
Mafuriko yaua watu karibu 40 Kongo DR
Nov 26, 2019 22:12Kwa akali watu 39 wamepoteza maisha kutokana na mafuriko katika mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kinshasa.
-
WHO yawahamisha karibu wafanyakazi 50 wa timu ya kupambana na Ebola huko Kongo kutokana na ukosefu wa usalama
Nov 26, 2019 09:30Shirika la Afya Duniani (WHO) limewahamisha wafanyakazi 49 miongoni mwa wale 120 waliokuwa katika timu ya kupambana na Ebola katika mji wa Beni nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kutokana na kuzorota kwa hali ya usalama. Hayo yamesemwa leo na msemaji wa WHO.