-
Idadi ya waliofariki dunia kwenye ajali ya ndege DRC yaongezeka + Sauti
Nov 25, 2019 12:06Idadi ya watu waliofariki dunia baada ya kuanguka ndege ndogo ya abiria katika mji wa Goma wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imeongezeka na kufikia watu 29 wakiwemo watu tisa wa familia moja. Watu wengine 19 wamejeruhiwa. Ndege hiyo iliyokuwa inaelekea Beni kutokea Goma ilianguka juu ya nyumba ya watu na kuua watu waliokuwemo ndani ya nyumba hiyo. Mossi Mwassi na maelezo zaidi
-
SAUTI, Wakazi wa Beni Kongo DR waandamana kuwataka askari wa Monusco kufanya kazi iliyowapeleka
Nov 23, 2019 12:52Wakazi wa Beni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamefanya maandamano makubwa wakilishinikiza jeshi la kusimamia amani la Umoja wa Mataifa MONUSCO kutekeleza wajibu wake wa kuwalinda raia wa nchi hiyo.
-
Wakazi wa Beni waandamana wakitaka askari wa MONUSCO waondoke DRC
Nov 22, 2019 23:11Wakazi wa mji wa Beni wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia wamefanya maandamano ya kushinikiza kuondoka nchini humo wanajeshi wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO.
-
WHO: Mapigano yanakwamisha mapambano dhidi ya Ebola Kongo DR
Nov 22, 2019 10:01Shirika la Afya Duniani (WHO) limetahadharisha kuwa, vita na mapigano huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yanakwamisha jitihada za kutokomeza ugonjwa hatari wa Ebola ambao umeua maelfu ya watu kufikia sasa.
-
Idadi ya waliouawa katika shambulizi la ADF nchini DRC yafika watu 15
Nov 17, 2019 04:12Idadi ya watu waliouawa katika shambulizi la kuvizia la kundi la wanamgambo wa ADF usiku wa kuamkia jana Jumamosi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imeongezeka na kufikia watu 15.
-
Wanamgambo wa ADF washambulia kijiji na kuua watu kadhaa Kongo DR
Nov 16, 2019 03:04Genge moja la wanamgambo limeshambulia kijiji kimoja na kuua watu sita wa familia moja mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Congo yaanza kutoa chanjo mpya ya Ebola katika mji wa Goma
Nov 14, 2019 21:55Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mpaka (MSF) imetangaza kuwa maafisa wa afya wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameanza kutoa chanjo mpya ya kudhibiti ugonjwa wa Ebola iliyotengenezwa na kampuni ya Johnson & Johnson.
-
Jeshi la Congo lamuua kiongozi wa tawi la waasi wa FDLR kutoka Rwanda
Nov 11, 2019 00:10Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo limetangaza kuwa limemuua kiongozi wa tawi lililojitenga la kundi la waasi wa Kihutu la Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR) mashariki mwa nchi hiyo.
-
Magaidi 25 wa ADF waangamizwa na jeshi la DRC mjini Beni
Nov 10, 2019 00:02Vikosi vya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo vimefanikiwa kuwaangamiza wapiganaji 25 wa kundi la wanamgambo wa ADF mashariki mwa nchi.
-
Ntaganda ahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kutenda jinai za kivita Congo DR
Nov 07, 2019 10:02Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela mbabe wa zamani wa vita katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Bosco Ntaganda baada ya kumpata na hatia ya kufanya ukatili ikiwa ni pamoja na kuua, kubaka na kuwatumikisha watoto kama askari vitani.