-
Watu 8 wauawa katika shambulizi mashariki mwa Kongo DR
Jan 08, 2019 11:09Kwa akali raia wanane wameuawa baada ya watu waliojizatiti kwa silaha kushambulia kijiji kimoja mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Uchaguzi DRC; CENI yatetea uamuzi wa kuakhirisha matokeo ya muda
Jan 06, 2019 04:46Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (CENI) imetetea uamuzi wake wa kuchelewesha matokeo ya muda ya uchaguzi wa rais uliofanyika Jumapili ya wiki iliyopita, ikisisitiza kuwa kufikia sasa haijaweza kuhesabu hata nusu ya kura zilizopigwa.
-
Hali ya wasiwasi yatanda DRC kabla ya matokeo ya uchaguzi
Jan 05, 2019 12:02Hali imeripotiwa kuwa tete katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Jumamosi hii, ikiwa yamesalia masaa machache kabla ya kutangazwa matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu wa wiki iliyopita.
-
Marekani yatumia kisingizio cha uchaguzi wa DRC kutuma askari Gabon
Jan 05, 2019 04:20Rais Donald Trump amesema Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) imetuma makumi ya askari wa nchi hiyo nchini Gabon, kwa ajili ya eti kuwalinda Wamarekani na ubalozi wa nchi hiyo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kufuatia uchaguzi mkuu wa wiki iliyopita katika nchi hiyo kubwa ya katikati mwa Afrika.
-
Viongozi wa kidini wataka kuheshimiwa matokeo ya kura DRC + Sauti
Jan 05, 2019 02:44Viongozi wa kidini wakiwemo wa Kanisa Katoliki huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya nchi hiyo kuheshimu matokeo ya kura na kumtangaza mshindi haraka iwezekanavyo. Mossi Mwasi na maelezo zaidi...
-
CENI: Matokeo ya muda ya uchaguzi wa DRC huenda yakacheleweshwa
Jan 03, 2019 11:52Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo CENI imesema yumkini italazimika kuchelewesha matokeo ya muda ya uchaguzi wa rais uliofanyika Jumapili iliyopita kutokana na sababu za kiufundi.
-
Zoezi la kuhesabu kura laendelea DRC, wapinzani walalamika + Sauti
Jan 03, 2019 04:27Huku zoezi la kuhesabu kura likiendelea katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, vyama vya upinzani vimekosoa mchakato huo baada ya kuripotiwa habari za kutupwa karatasi za kupigia kura za mgombea wa upinzani katika baadhi ya maeneo. Mossi Mwasi na maelezo zaidi...
-
SADC yaubariki uchaguzi wa Kongo DR licha ya ghasia na malalamiko
Jan 02, 2019 23:42Huku zoezi la kuhesabu kura likiendelea katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, timu ya waangalizi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) imesema uchaguzi mkuu wa Jumapili iliyopita nchini humo ulifanyika vizuri kwa kiasi kikubwa.
-
Msalaba Mwekundu: Mamia ya Wakongomani wamekimbilia Uganda
Jan 02, 2019 11:46Shirika la Msalaba Mwekundu limesema mamia ya raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamekimbilia nchini Uganda baada ya kufanyika uchaguzi mkuu wa Jumapili iliyopita.
-
Zoezi la kuhesabu kura laendelea DRC
Jan 02, 2019 04:16Zoezi la kuhesabu kura linaendelea katika maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo huku huduma ya intaneti na ujumbe mfupi wa simu za mkononi (SMS) zikiwa bado zimekatwa kote nchini humo.