• Kongo yakata huduma ya intaneti kwa siku ya pili kuzuia machafuko kabla ya matokeo ya uchaguzi

    Kongo yakata huduma ya intaneti kwa siku ya pili kuzuia machafuko kabla ya matokeo ya uchaguzi

    Jan 01, 2019 11:45

    Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imekata huduma ya intaneti na ujumbe wa mfupi wa simu za mkononi wa SMS kote nchini humo kwa siku ya pili mfululizo hii leo wakati nchi hiyo ikisubiri kwa hamu kubwa matokeo ya kwanza ya uchaguzi wa Rais.

  • Wapinzani Kongo DR walalamikia ukiukwaji mkubwa wa taratibu katika uchaguzi wa rais

    Wapinzani Kongo DR walalamikia ukiukwaji mkubwa wa taratibu katika uchaguzi wa rais

    Dec 31, 2018 04:35

    Wagombea wakuu wa upinzani katika uchaguzi wa rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamedai kuwa uchaguzi wa jana Jumapili ulikumbwa na changamoto nyingi, zikiwemo za kukwama kwa mashine za kupigia kura, mvua kubwa katika maeneo mengi pamoja na machafuko na vurugu.

  • Uchaguzi DRC: Wakazi wa Beni wafanya uchaguzi wa mwigo

    Uchaguzi DRC: Wakazi wa Beni wafanya uchaguzi wa mwigo

    Dec 30, 2018 11:45

    Licha ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo CENI kuakhirisha uchaguzi katika maeneo matatu ya nchi hiyo ya Beni, Butembo na Yumbi kutokana na ugonjwa wa Ebola na mapigano ya kikabila, lakini maelfu ya wakazi wa mji wa Beni hii leo wamepanga foleni na kushiriki uchaguzi wa mwigo, wakiwa na lengo la kuidhihaki tume hiyo.

  • Uchaguzi Mkuu DRC katikati ya changamoto za kiusalama na mivutano ya kisiasa

    Uchaguzi Mkuu DRC katikati ya changamoto za kiusalama na mivutano ya kisiasa

    Dec 30, 2018 10:10

    Uchaguzi Mkuu wa Rais na Bunge wa Jamhuri ya Kidemokrsia ya Kongo umefanyika leo Jumapili Disemba 30, 2018 huku mvua kali ikinyesha. Uchaguzi huo umefanyika chini ya changamoto nyingi za kiusalama na kisiasa.

  • Uchaguzi wa rais ulioakhirishwa kwa muda mrefu waanza Kongo

    Uchaguzi wa rais ulioakhirishwa kwa muda mrefu waanza Kongo

    Dec 30, 2018 04:36

    Raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kong leo Jumapili wameelekea kwenye masanduku ya kupigia kura katika uchaguzi wa rais ulioakhirishwa kwa muda mrefu nchini humo. Uchaguzi huo wa leo huwenda ukawa wa kwanza wa kukabidhiana madaraka kwa njia ya kidemokrasia katika nchi hiyo iliyokumbwa na machafuko.

  • Uchaguzi mkuu wa Kongo na changamoto zinazoikabili nchi hiyo

    Uchaguzi mkuu wa Kongo na changamoto zinazoikabili nchi hiyo

    Dec 29, 2018 07:39

    Uchaguzi mkuu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hatimaye utafanyika kesho Jumapili baada ya kuakhirishwa mara kadhaa. Raia wa nchi hiyo kesho Jumapili tarehe 30 Disemba wataelekea kwenye masanduku ya kupigia kura kumchagua mrithi wa Rais Joseph Kabila licha ya kuendelea mivutano ya kisiasa nchini humo.

  • Katibu Mkuu wa UN ataka uchaguzi huru na wa haki Kongo DR

    Katibu Mkuu wa UN ataka uchaguzi huru na wa haki Kongo DR

    Dec 29, 2018 04:45

    Huku wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo waliotimiza masharti ya kupiga kura wakitazamiwa kuelekea katika masanduku ya kupigia kura kumchangua kiongozi atakayerithi mikoba ya Rais Joseph Kabila Jumapili ya kesho, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa mwito kwa pande zote husika za kisiasa kuhakikisha kuwa zoezi hilo linafanyika kwa uhuru na amani.

  • Martin Fayulu, mgombea wa upinzani aongoza katika kura ya maoni DRC

    Martin Fayulu, mgombea wa upinzani aongoza katika kura ya maoni DRC

    Dec 28, 2018 12:34

    Utafiti mpya wa maoni umeonesha kuwa mgombea wa muungano wa upinzani wa Lamuka katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Martin Fayulu ndiye mwenye nafasi kubwa ya kuibuka mshindi katika uchaguzi wa rais unaotazamiwa kufanyika Jumapili ijayo.

  • Wagonjwa 24 wa Ebola watoroka kituo cha matibabu Beni, Kongo DR

    Wagonjwa 24 wa Ebola watoroka kituo cha matibabu Beni, Kongo DR

    Dec 27, 2018 23:33

    Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetangaza habari ya wagonjwa 24 walioambukizwa ugonjwa hatari wa Ebola kutoroka kituo cha matibabu mjini Beni, mashariki mwa nchi.

  • Wapinzani kongo DR waendelea kuilalamikia tume ya uchaguzi CENI + Sauti

    Wapinzani kongo DR waendelea kuilalamikia tume ya uchaguzi CENI + Sauti

    Dec 27, 2018 23:19

    Vyama vya upinzani vya Jamhuri ya Kidemokrsia ya Kongo vimeendelea kukosoa hatua ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya nchi hiyo CENI ya kuakhirisha uchaguzi katika miji mitatu nchini humo. Uchaguzi Mkuu wa Rais na Bunge unatarajiwa kufanyika Jumapili hii DRC, lakini hautofanyika katika miji ya Yumbi, Beni na Butembo hadi tarehe 30 Machi mwakani. Mossi Mwasi na maelezo zaidi...