-
Polisi Kongo DR yajiweka tayari kuzima maandamano dhidi ya Kabila
Jan 21, 2018 04:05Maafisa wa polisi wameonekana wakilinda doria katika kila kona ya mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kinshasa, masaa machache kabla ya kuanza maandamano ya kumshinikizi Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo aachie ngazi.
-
Museveni aituhumu UN kuwa 'inalinda ugaidi' Kongo DR
Jan 17, 2018 11:14Rais Yoweri Museveni wa Uganda ameibua tuhuma nzito dhidi ya Umoja wa Mataifa akidai kuwa chombo hicho cha kimataifa 'kinalinda ugaidi' mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Jeshi la Kongo lazindua operesheni dhidi ya waasi wa ADF wa Uganda
Jan 14, 2018 04:19Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limeanzisha operesheni kali dhidi ya kundi la ADF la Uganda katika mji wa Beni mashariki mwa nchi.
-
UN yataka kufanyika uchunguzi kuhusu ghasia za karibuni nchini Kongo
Jan 10, 2018 04:08Umoja wa Mataifa umetaka kufanyika uchunguzi kuhusu ghasia zilizoikumba Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mwezi Disemba mwaka jana.
-
Kuenea mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu Kongo
Jan 08, 2018 04:49Maafisa wa afya nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamearifu kuenea mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu huko Kinshasa mji mkuu wa nchi hiyo kufuatia mafuriko yaliyoikumba nchi hiyo.
-
Kanisa Katoliki Kongo DR lalaani vikali ukandamizaji wa polisi dhidi ya wafuasi wake
Jan 05, 2018 04:32Kanisa Katoliki nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limelaani vikali vitendo vya ukatili na ukandamizaji walivyofanyiwa watu waliokuwa wamekusanyika kwa ajili ya shughuli ya kidini katika mji mkuu wa nchi hiyo, Kinshasa.
-
Umoja wa Ulaya wakosoa ukandamizaji wa serikali ya Congo DR dhidi ya wapinzani
Jan 03, 2018 23:43Umoja wa Ulaya umewatuhumu maafisa wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuwa wanakabiliana kwa mabavu na matakwa ya wananchi wanaosisitiza udharura wa kuondoka madarakani rais wa sasa wa nchi hiyo.
-
Katibu Mkuu wa UN amtaka Rais wa Kongo atimize ahadi ya kuondoka madarakani
Jan 01, 2018 12:49Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amemtaka Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo aheshimu makubaliano yanayomtaka ang'atuke madarakani. Antonio Guterres ameyasema hayo baada ya kuuliwa watu wanane katika maandamano yaliyofanyika jana dhidi ya utawala wa Rais Kabila.
-
Kadhaa wauawa katika maandamano dhidi ya serikali Kongo DR
Dec 31, 2017 11:09Kwa akali watu wawili wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika ghasia za maandamano dhidi ya serikali katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Makundi ya waasi yazidi kusakamwa, wapiganaji 6 wa Mai-Mai wauawa DRC
Dec 29, 2017 04:20Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limetangaza habari ya kuua wanachama sita wa kundi la waasi wa Mai-Mai katika eneo la Kasindi mkoani Kivu Kaskazini, siku chache baada ya wapiganaji hao kuteketeza moto nyumba ya Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo katika mji wa Musienene katika mkoa huo.