-
Kipindupindu chauwa watu 50 Kongo katika muda wa wiki moja
Nov 19, 2017 12:40Mratibu wa Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ugonjwa wa Kipindupindu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametangaza kuwa watu 50 wamefariki dunia nchini humo baada ya kuambukizwa ugonjwa huo katika muda wa wiki moja.
-
Polisi ya Kongo DR yawafyatulia risasi wapinzani na kujeruhi kadhaa kati yao Kinshasa
Nov 19, 2017 00:55Jeshi la polisi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limetumia mtutu wa chuma kuwafyatulia risasi wafuasi wa upinzani dhidi ya Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo, na kupelekea watu kadhaa kujeruhiwa katika mji mkuu wa nchi hiyo, Kinshasa.
-
Tahadhari ya kuuawa wanajeshi zaidi kaskazini mashariki mwa DRC
Nov 17, 2017 00:42Mkuu wa jumuiya moja ya kijamii ya kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametahadharisha kuhusu kuongezeka mauaji ya wanajeshi wa nchi hiyo wanaouliwa na waasi.
-
Watu 18 wakabiliwa na tuhuma za kufanya ukatili wa kingono Congo DR
Nov 14, 2017 12:22Watu 18 akiwemo afisa mmoja wa serikali ya kikanda wanakabiliwa na tuhuma za kufanya ukatili wa kingono huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
Watu 33 wapoteza maisha katika ajali ya treni ya mizigo DRC
Nov 13, 2017 12:13Watu 33 wamepoteza maisha siku ya Jumapili asubuhi, tarehe 12 Novemba, katika mkoa wa Lualaba wa kusini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, baada ya kutokea ajali ya treni ya mizigo ambayo imepelekea kujeruhiwa pia watu wengine kadhaa miongoni mwa abiria haramu karibu na mji wa Buyofwe.
-
SAUTI, Kiwanda cha kuzalisha umeme mji wa Kisangani Kongo DR, chazingirwa na mafuriko, mji wawa totoro
Nov 11, 2017 12:17Athari ya mvua zinazoendelea kunyesha katika nchi kadhaa za Afrika zimeendelea kushuhudiwa ambapo mbali na kusababisha maafa zimesababisha pia uharibifu wa miundombinu.
-
UN yaitaka Kongo kuitisha uchaguzi na kusafisha taswira yake ya haki za binadamu
Nov 10, 2017 03:58Kamati ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imeipatia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo muhula wa mwaka mmoja kuripoti kuhusu hatua ilizochukua ili kuhakikisha kuwa inaitisha uchaguzi huru na wa kiadilifu sambamba na kusafisha rekodi yake ya haki za binadamu.
-
Umoja wa Mataifa wataka kukamatwa watu waliouwa wataalamu wake Congo DR
Nov 10, 2017 00:50Umoja wa Mataifa umeitaka serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kutoa ushirikiano katika jitihada za kuweka wazi kadhia ya mauaji ya wataalamu wake wawili nchini humo.
-
Wakimbizi wa Kongo DR wadai kuwa jeshi linaua na kubaka raia
Nov 09, 2017 04:17Maelfu ya wakimbizi raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo waliokimbilia nchi jirani ya Zambia wamelituhumu jeshi la nchi yao kuwa linahusika na mauaji na ubakaji dhidi yao.
-
Upinzani Kongo DR wapinga tarehe ya uchaguzi iliyotangazwa na CENI
Nov 06, 2017 23:14Vyama vya upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo vimepinga tarehe ya uchaguzi iliyopendekezwa na Tume ya Uchaguzi CENI hivi karibuni.