Feb 06, 2023 07:41
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani vikali shambulio lililofanywa Jumapili huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC dhidi ya helikopta ya ujumbe wa umoja huo wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO, shambulio ambalo limesababisha kifo cha mlinda amani mmoja wa UN kutoka Afrika Kusini na mwingine kujeruhiwa.