-
Tanzania yazuia safari za Kenya Airways nchini humo
Jul 31, 2020 23:33Tanzania imesimamisha shirika la ndege la Kenya (KQ) kufanya safari za kwenda Tanzania kuanzia leo tarehe Mosi Agosti, siku moja baada ya Kenya kutangaza kuwa itafungua anga zake kwa usafiri wa kimataifa isipokuwa kutoka baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania.
-
Rais wa Kenya atangaza kurefusha muda wa kafyu kukabiliana na Covid-19
Jul 27, 2020 12:23Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya leo Jumatatu amerefusha kipindi cha kafyu nchini humo kwa siku nyingine 30 na kupiga marufuku uuzaji wa pombe migahawani ili kuzuia maambukizi ya COVID-19 nchini humo.
-
EABC yazitaka nchi zote za Afrika Mashariki kufungua anga zao, kuruhusu utalii na biashara
Jul 14, 2020 08:38Baraza la Biashara la Nchi za Afrika Mashariki (EABC), limezisihi nchi zote za kanda hiyo kufuata mfano wa Tanzania kwa kufungua anga zao ili kuruhusu safari za kimataifa kuingia na kutoka katika nchi zote za kanda hiyo.
-
Wasomi, wanachuo wa Kenya nchini Marekani wakosoa agizo la Trump dhidi yao
Jul 11, 2020 10:18Wahadhiri na wanachuo raia wa Kenya walioko Marekani wamekosoa vikali agizo lililotolewa na rais wa nchi hiyo, Donald Trump, la kutaka wanafunzi wote wa kigeni waondoke nchini humo ndani ya miezi miwili ijayo.
-
Kenya ni nchi ya kwanza Afrika kusambaza intaneti kupitia baluni
Jul 08, 2020 11:35Kenya imekuwa nchi ya kwanza kutoa huduma za inteneti kupitia baloni (puto) na hivyo kuwawezesha maelfu ya watu nchini humo kupata huduma za intaneti kirahisi.
-
Rais Kenyatta alegeza hatua kwa hatua sheria za kukabiliana na corona Kenya
Jul 06, 2020 06:55Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amelegeza kwa kiasi fulani sheria kali zilizokuwa zimewekwa kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19 ambapo umeua watu 150 kufikia sasa nchini humo.
-
Wananchi wa Kenya waandamana kulaani ukatili wa polisi ya nchi hiyo
Jun 09, 2020 03:36Wananchi wa Kenya wamefanya maandamano katika mji mkuu Nairobi, kulaani ukandamizaji na ukatili wa polisi ya nchi hiyo dhidi ya raia.
-
Maandamano ya kulaani ukatili wa polisi ya Marekani yafanyika Kenya, Nigeria
Jun 02, 2020 23:26Miji mikuu ya Kenya na Nigeria jana ilishuhudia maandamano ya kulaani ubaguzi wa rangi na mauaji ya George Floyd, raia wa Marekani mwenye asili ya Afrika aliyeuliwa kikatili na polisi mmoja mzungu katika mji wa Minneapolis, katika jimbo la Minnesota nchini Marekani wiki iliyopita.
-
SAUTI, Raia wa Kenya wakasirishwa na tabia ya Shirika la Umeme la nchi hiyo (Kenya Power) kukatakata huduma hiyo
May 09, 2020 10:26Shirika la Kusambaza Umeme nchini Kenya (Kenya Power), limetuhumiwa kwa kufanya uzembe mkubwa katika utoaji huduma za umeme kwa raia wa nchi hiyo huku wananchi wengi wakiitaka serikali kutoa vibali kwa makampuni mengine kuanza kuusambaza umeme ili kuleta ushindani wa kibiashara.
-
Ethiopia yakiri kutungua ndege ya Kenya katika ardhi ya Somalia
May 09, 2020 08:05Askari wa jeshi la Ethiopia wamekiri kuwa walitungua kimakosa ndege ndogo ya Kenya iliyokuwa imebeba misaada na vifaa vya kupambana na janga la corona katika mji wa Bardale, kusini mwa eneo la Bay nchini Somalia.