-
KDF yashambulia ngome za al-Shabaab karibu na Afmadow, Somalia
Aug 10, 2017 10:15Ndege za Jeshi la Ulinzi la Kenya KDF zimeshambulia ngome za kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab katika eneo la Weelmarow karibu na wilaya ya Afmadow, eneo la Lower Juba, kusini mwa Somalia.
-
Wakenya watakiwa kudumisha amani; waangalizi wataka madai ya upinzani kuchunguzwa
Aug 10, 2017 10:09Waangalizi wa kimataifa wa uchaguzi wa Kenya uliofanyika siku ya Jumanne wametoa wito na kuwataka wananchi wa nchi hiyo ya Afrika Mashariki kudumisha amani na utulivu.
-
Watu 5 wameuawa katika ghasia za baada ya uchaguzi mkuu Kenya
Aug 10, 2017 04:18Watu 5 wameripotiwa kuuawa katika ghasia na machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika juzi nchini Kenya baada ya kinara wa kambi ya upinzani, Raila Odinga kudai kuwa kumefanyika udanganyifu mkubwa.
-
Igad: Uchaguzi mkuu Kenya umefanyika kwa amani, uwazi na utaratibu sahihi
Aug 09, 2017 11:41Timu ya wasimamizi wa uchaguzi ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiserikali wa Nchi za Mashariki na Pembe ya Afrika (Igad) imeipongeza Tume Huru ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC) kwa kusimamia uchaguzi kwa njia sahihi na kusema kuwa, tume hiyo inapaswa kuwa kigezo cha kuigwa na nchi nyingine za Afrika.
-
Kaimu Waziri wa Usalama wa Ndani Kenya awaonya wanaoeneza ujumbe wa chuki mitandaoni
Aug 09, 2017 11:03Kaimu Waziri wa Usalama wa Ndani wa Kenya amewaonya watu wanaoeneza ujumbe wa chuki katika mitandao ya kijamii na kusambaza ripoti au taarifa zinazotishia usalama wa taifa.
-
Ngombea Urais akiri kushindwa Kenya, mmoja auawa kituo cha uchaguzi Kisii
Aug 09, 2017 10:29Mgombea urais wa kujitegemea katika uchaguzi mkuu wa Kenya amekiri kushindwa baada ya matokeo ya awali ya uchaguzi wa rais kuonesha kuwa, ameshika nafasi ya sita kwa kupata kura elfu 11 na 256.
-
Uhuru Kenyatta aongoza katika uchaguzi wa rais Kenya, upinzani wapinga matokeo
Aug 08, 2017 22:58Kinara wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amepinga matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais uliofanyika jana Jumanne, yanayoonyesha kuwa Rais wa sasa Uhuru Kenyatta anaongoza.
-
SAUTI, Matukio ya uchaguzi mkuu nchini Kenya
Aug 08, 2017 12:38Mamilioni ya Wakenya leo wameshiriki kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, madiwani, maseneta, wabunge, magavana na wawakilishi wa wanawake.
-
Uchaguzi mkuu wa Kenya wafanyika katika hali ya msisimko wa kipekee
Aug 08, 2017 11:59Mamilioni ya Wakenya leo wameshiriki kwenye uchaguzi mkuu wa kumchagua Rais, madiwani, maseneta, wabunge, magavana na wawakilishi wa wanawake.
-
UN: Tunafuatilia kwa karibu uchaguzi wa Kenya
Aug 08, 2017 03:21Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema umoja huo unafuatilia kwa karibu zoezi la uchaguzi mkuu linalofanyika hii leo nchini Kenya.