-
Igad yataka kufanyika uchaguzi wa amani Kenya
Aug 08, 2017 00:09Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiserikali wa Nchi za Mashariki na Pembe ya Afrika (Igad) imewatolea wito washika dau wote katika uchaguzi mkuu wa Kenya kuhakikisha kuwa uchaguzi wa leo unafanyika kwa amani na utulivu.
-
Wakenya wakusanya akiba ya chakula kabla ya uchaguzi mkuu kesho Jumanne
Aug 07, 2017 12:11Wananchi wa Kenya ambao wamejawa na wasiwasi leo wamekuwa wakikusanya na kujiwekea akiba ya chakula huku polisi wakiwa tayari wameandaa masanduku ya huduma ya kwanza siku moja kabla ya uchaguzi mku wa kesho ambao wengi wanahofu kwamba huwenda ukaitumbukiza tena nchi hiyo katika hali ya mchafukoge.
-
Le Monde: Baadhi ya Wakenya wanakimbia makazi yao kwa kuogopa machafuko ya uchaguzi
Aug 05, 2017 23:16Kumbukumbu chungu na mbaya za uchaguzi wa rais wa mwaka 2007 nchini Kenya zinawalazimisha baadhi ya raia wa nchi hiyo kukimbia makazi na miji yao.
-
Kenya yamtimua mtaalamu wa data za uchaguzi wa Marekani, alifanya kazi na NASA
Aug 05, 2017 09:58Polisi ya Kenya uimemtia nguvuni na kumtimua nchini humo mtaalamu wa data za uchaguzi wa Marekani na mwenzake wa Canada waliokuwa wakifanya kazi na muungano wa upinzani wa Nasa, zikiwa zimesalia siku kadhaa kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 8.
-
AU: Wakenya wanataka uchaguzi huru, wa haki na wenye uwazi
Aug 05, 2017 03:41Rais wa zamani wa Afrika Kusini ambaye anaongoza timu ya waangalizi wa uchaguzi wa Umoja wa Afrika AU nchini Kenya amesema wananchi wa taifa hilo la Afrika Mashariki wanataka kuona zoezi hilo la Jumanne ijayo linafanyika katika mazingira huru, yenye haki na uwazi.
-
Al-Shabaab washadidisha hujuma kabla ya uchaguzi, waua watu 4 Kenya
Aug 03, 2017 02:52Huku uchaguzi mkuu wa Agosti 8 ukizidi kujongea nchini Kenya, kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab linaonekana kushadidisha mashambulizi yake dhidi ya raia na maafisa usalama wa nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
-
Hali ya wasiwasi yashtadi katika kukaribia uchaguzi mkuu Kenya
Aug 02, 2017 09:57Hali ya wasiwasi imeongezeka huko Kenya ikiwa zimesalia siku chache hadi kufanyika uchaguzi mkuu nchini humo tarehe 8 Agosti.
-
Wawili waliuawa katika shambulio nyumbani kwa Makamu wa Rais wa Kenya
Jul 31, 2017 10:52Watu wawili waliuawa juzi katika shambulio lililofanywa katika makazi ya Makamu wa Rais wa Kenya, William Rutto. Hayo yameelezwa na polisi siku kadhaa kabla ya nchi hiyo ya Kiafrika kuendesha uchaguzi wa Rais tarehe nane Agosti.
-
SAUTI, Ripoti ya matukio ya Kiislamu kuanzia kilio cha Waislamu Kenya, Uganda na ongezeko la talaka za kiholela Zanzibar
Jul 29, 2017 10:54Ripoti ya matukio ya Kiislamu kuanzia malalamiko ya Waislamu kwa ofisi ya uhamiaji nchini Kenya ambayo inatajwa kufanya makusudi kuchelewesha kuwapatia pasi za kusafiria Waislamu zaidi ya 100 wanaotaka kwenda kushiriki ibada ya Hijja ya mwaka huu huo Saudia.
-
Makazi ya Makamu wa Rais Kenya, William Ruto yavamiwa na watu wenye silaha
Jul 29, 2017 09:03Watu wenye silaha wasiojulikana wamevamia leo nchana nyumba ya Makamu wa Rais nchini Kenya William Ruto katika eneo la Sugoi, Kaunti ya Uasin Gishu.