-
UN yazipongeza pande hasimu Libya kwa kuafikiana kufanyika uchaguzi
Nov 12, 2020 07:30Umoja wa Mataifa umepongeza hatua ya pande hasimu za kisiasa nchini Libya kukubaliana kuitisha uchaguzi mkuu nchini humo katika kipindi cha miezi 18 ijayo.
-
Haftar aamua kuvunja makundi ya wanamgambo mkoani Benghazi
Nov 09, 2020 04:42Kundi linalojiiita jeshi la kitaifa la Libya linaloongozwa na Khalifa Haftar limetangaza kuwa limeandaa mpango wa kuyavunja makundi yenye silaha na kuondoka katika makazi yake katika mkoa wai Benghazi nchini humo.
-
Makaburi zaidi ya umati yagunduliwa Libya
Nov 08, 2020 07:59Miili ya watu 17 imegunduliwa katika kaburi la umati huko magharibi mwa Libya, mkoani Tarhuna, na hivyo kufanya jumla ya miili iliyofukuliwa katika miezi ya hivi karibuni kufikia 112.
-
Wafanyakazi wa Sudan nchini UAE wanahadaiwa kuingia vitani Libya
Nov 06, 2020 10:43Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limefichua kuwa mamia ya raia wa Sudan wanaofanya kazi katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) wamehadaiwa kuingia vitani Libya na kujiunga na wanamgambo wa jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
UN: Mazungumzo ya amani Libya yanaendelea kwa mafanikio huko Ghadames
Nov 03, 2020 08:53Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa mazungumzo ya pande hasimu nchini Libya yanayoendelea katika mji wa Ghadames ulioko kusini magharibi mwa nchi hiyo yamepiga hatua kubwa katka njia ya kufikia makubaliano juu ya utekelezaji wa mapatano ya kusitisha vita yaliyotiwa saini wiki kadhaa zilizopita.
-
HRW: Imarati imetuma mamia ya vijana wa Kisudan kupigana vita Libya
Nov 03, 2020 02:46Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch lenye makao yake makuu mjini New York nchini Marekani limetangaza kuwa, kampuni ya huduma za ulinzi na usalama ya Black Shield ya Imarati iliajiri karibu vijana 270 za Kisudani kwa ajili ya kufanya kazi za ulinzi katika Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) lakini vijana hao walijikuta wakitumwa Libya kwenda kupigana katika safu za jenerali muasi, Khalifa Haftar.
-
Libya yamtaka Rais wa Ufaransa awaombe radhi Waislamu kwa kumvunjia heshima Mtume (saw)
Oct 30, 2020 06:40Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa nchini Libya imelaani matamshi yaliyotolewa na Rais Emanuel Macron wa Ufaransa akimvunjia heshima Mtume wa Mwenyezi Mungu, Muhammad (saw) na kumtaka awaombe radhi Waislamu
-
Libya yamtaka Macron awaombe radhi Waislamu duniani
Oct 27, 2020 03:13Wizara ya Mambo ya Nje ya Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya imelaani matamshi ya rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ya kumvunjia heshima Mtume Muhammad SAW na Uislamu na kumtaka afanye haraka kuwaomba radhi Waislamu duniani.
-
Wahamiaji 11 akiwemo mjamzito wafa maji Libya wakielekea Ulaya
Oct 26, 2020 11:40Wahajiri 11 akiwemo mwanamke mjamzito wamefariki dunia katika Bahari ya Mediterania baada ya boti yao kuzama, huko pwani ya Libya.
-
Umoja wa Afrika wapongeza makubaliano ya kusitisha vita nchini Libya
Oct 25, 2020 12:12Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amepongeza makubaliano ya kukomesha vita na mapigano nchini Libya akiyataja kuwa ni hatua muhimu katika njia ya kurejesha amani katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.