-
Serikali ya mwafaka wa kitaifa ya Libya yataka kukatwa uhusiano na Imarati
May 16, 2020 11:02Mjumbe wa Baraza la Rais la Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa nchini Libya, sambamba na kuashiria ripoti ya siri ya Umoja wa Mataifa kuhusiana na uungaji mkono wa Imarati kwa jenerali muasi Khalifa Haftar, ametaka kukatwa uhusiano wa Tripoli na Abu Dhabi.
-
Kupamba moto mgogoro Libya na uingiliaji wa maajinabi katika masuala ya ndani ya nchi hiyo
May 13, 2020 11:44Mapigano ya ndani nchini Libya yamepamba moto hivi sasa na kutoa fursa kwa madola ajinabi yanayojali maslahi yao binafsi tu, kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo.
-
Onyo la Uturuki dhidi ya vikosi vyenye mfungamano na Saudi Arabia nchini Libya
May 12, 2020 10:07Uwepo wa kijeshi wa Uturuki nchini Libya na vita vya niaba vya Ankara dhidi ya baadhi ya madola ya Kiarabu yenye fikra mgando kama Saudi Arabia, kumeshadidisha matatizo ya serikali ya Recep Tayyip Erdogan barani Afrika.
-
Uturuki: Taarifa ya nchi tano dhidi yetu imetumia vipimo vya kiundumakuwili
May 12, 2020 07:40Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki imesema, taarifa ya pamoja iliyotolewa na Misri, Ugiriki, Imarati, Ufaransa na Cyprus kuhusu Bahari ya Mediterania inaonyesha vipimo vya kiundumakuwili vinavyotumiwa na nchi hizo.
-
Spika wa Bunge la Libya: Khalifa Haftar hatokuwa mshirika wetu wa kisiasa hapo baadaye
May 12, 2020 02:41Spika wa bunge la Libya amebainisha kwamba, serikali ya Tripoli haimtambui Jenerali Khalifa Haftar kuwa mshirika wake wa kisiasa wa baadaye.
-
Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya: Tumekiharibu kikamilifu kituo cha anga cha Haftar
May 11, 2020 08:08Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya (GNA) imetangaza kuwa, mashambulio ya anga yaliyofanywa na vikosi vyake yamekiharibu kikamilifu kituo cha anga cha vikosi vinavyoongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Tunisia yaisaidia Uturuki kufikisha misaada Libya
May 09, 2020 00:00Serikali ya Tunisia imeiruhusu ndege ya Uturuki ambayo inasemekana ilikuwa na misaada ya kitiba kwa ajili ya Libyan itue nchini humo.
-
Wanamgambo wa Haftar waendelea kudondosha mabomu na kuua raia Libya
May 08, 2020 08:13Wanamgambo wanaojiita Jeshi la Taifa la Libya wanaoogozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar wameendelea kutekeleza mashambulizi mtawalia ya mabomu katika mji mkuu Tripoli, licha ya janga la corona na mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Guterres aelezea hofu yake kutokana kushiriki mamluki katika vita Libya
May 07, 2020 13:05Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameelezea hofu kubwa aliyo nayo kutokana na kutumiwa mamluki katika vita vya Libya.
-
Wanamgambo wa Haftar: Tumeua askari 40 wa Serikali ya Libya
May 06, 2020 07:52Wanamgambo wanaojiita Jeshi la Taifa la Libya wanaoogozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar wanadai wametekeleza operesheni kali iliyoua askari 40 wa Jeshi la Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa inayoongozwa na Waziri Mkuu, Fayez al-Sarraj.