-
Serikali ya Canada yahukumiwa kuwalipa fidia wakazi asili wa nchi hiyo
Oct 01, 2021 01:41Mahakama ya Haki za Binadamu ya Canada ambayo mwaka 2016 iliituhumu serikali ya nchi kuwa imefanya ubaguzi wa kimbari, kutumia mabavu na kuua Wahindi Wekundu wenyeji wa nchi hiyo imeitaka serikali ya Ottawa kuwalipa fidia Wahindi Wekundu kwa kupatikana na hatia ya kukiuka haki zao za kibinadamu
-
Palestina yataka kuharakishwa kesi ya kuchunguza uhalifu wa Israel mahakama ya ICC
Sep 05, 2021 02:49Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Palestina imetoa wito wa kuharakishwa mwenendo wa kesi ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) huko Hague nchini Uholanzi kwa ajili ya kuchunguza jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina.
-
Wafuasi wa chama cha upinzani Tanzania Chadema wakamatwa wakiimba "Mbowe sio gaidi"
Aug 05, 2021 08:03Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambacho ni chama kikuu cha upinzani Tanzania waliokuwa wamekusanyika nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kuzuiwa kuingia ndani ya korti wamekamatwa na wanashikiliwa na Jeshi la Polisi.
-
Wanasheria Tanzania wataka Mbowe ama aachiwe au afikishwe mbele vyombo vya sheria
Jul 25, 2021 06:59Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kimeingilia kati sakata la kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, kikitaka kiongozi huyo wa upinzani Tanzania ama aachiliwe huru au afikishwe kwenye mamlaka za kisheria.
-
Mahakama Afrika Kusini yamhukumu Zuma zaidi ya mwaka mmoja jela
Jun 29, 2021 21:55Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ambaye kesi yake ya ufisadi inaendelea, amehukumiwa kifungo cha miezi 15 gerezani kwa kudharau korti.
-
Askari polisi aliyemuua Mmarekani mweusi, George Floyd apatikana na hatia
Apr 21, 2021 01:29Derek Chauvin, afisa mzungu wa polisi wa Marekani ambaye alimuua kikatili Mmarekani mwenye asili ya Afrika, George Floyd na kuzusha maandamano makubwa ya kupinga ubaguzi wa rangi dunia nzima hatimaye amepatikana na hatia katika mashitaka yote ya mauaji yaliyokuwa yakimuandama.
-
Waziri Mkuu wa zamani wa Kuwait azuiwa kusafiri nje ya nchi kwa tuhuma za ufisadi
Mar 30, 2021 03:32Mahakama ya Mawaziri inchini Kuwait imempiga marufuku kusafiri nje ya nchi Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo. Jaber al Mubarak al Hamad all Sabah anakabiliwa na kesi ya ufisadi wa mamia ya mamilioni ya dinari za mfuko wa hazina wa jeshi la nchi hiyo.
-
Mahakama ya Katiba ya Niger 'yabariki' ushindi wa Mohamed Bazoum
Mar 22, 2021 06:43Mahakama ya Katiba ya Niger imeidhinisha ushindi wa matokeo ya uchaguzi wa rais yaliyompa ushindi mgombea wa chama tawala cha PNDS, Mohamed Bazoum.
-
Kesi ya uchaguzi; Mahakama ya Juu ya Uganda yakataa ombi la Wine
Feb 09, 2021 23:01Mahakama ya Juu ya Uganda imetupilia mbali ombi la mwanasiasa wa upinzani nchini Uganda Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, la kutaka kufanyia marekebisho faili lake la kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais yaliyompa ushindi Rais Yoweri Museveni.
-
Mmishonari wa Marekani afungwa miaka 15 kwa kunajisi mayatima Kenya
Feb 05, 2021 08:15Raia wa Marekani ambaye alikuwa anafanya kazi kama mmishonari nchini Kenya amehukumiwa kifungo cha zaidi ya miaka 15 jela, baada ya kupatikana na hatia ya kuwanajisi mabinti mayatima.