-
Chama cha Fat'h: Marekani inashirikiana na Israel kuwakandamiza Wapalestina
Feb 25, 2022 03:25Katibu wa Kamati Kuu ya chama cha Fat'h cha Palestina amesema kuwa, eneo la Sheikh Jarrah na maeneo mengine ya Quds yanayokaliwa kwa mabavu, yanaendelea kushuhudia vitendo vya kigaidi vya utawala wa Kizayuni wa Israel na kwamba jinai hizo zinafanyika kwa uungaji mkono kamili wa Marekani.
-
Takwimu: Vifo vya uzazi vimeongezeka Marekani kutokana na ubaguzi wa rangi
Feb 24, 2022 09:05Vifo vya uzazi vya akina mama nchini Marekani, ambayo ndiyo inavyoongoza kwa sasa duniani, vilifikia kiwango cha juu zaidi katika nusu karne mwaka wa 2020, na uwezekano wa kufariki dunia wanawake weusi wenye asili ya Afrika raia wa Marekani ni mara tatu zaidi ya wanawake wa kizungu.
-
Iran: Uingiliaji wa US, NATO umeshadidisha mgogoro wa Ukraine
Feb 22, 2022 23:12Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekosoa vikali chokochoko za Marekani na shirika la kijeshi la NATO katika mgogoro wa Ukraine na kusisitiza kuwa, uingiliaji huo umeshadidisha taharuki mashariki mwa nchi hiyo jirani na Russia.
-
Msimamo wa mwakilishi maalumu wa Marekani katika masuala ya Afghanistan kuhusu kuendelezwa diplomasia na Taliban
Feb 22, 2022 11:14Baada ya kupita miezi sita tangu wanamgambo wa Taliban wachukue madaraka nchini Afghanistan, mjumbe maalumu wa Marekani katika masuala ya Afghanistan amesema kuwa, kuendelezwa mawasiliano na Taliban na kufanyika mazungumzo baina ya Waafghani ndio chaguo bora zaidi na ni kwa maslahi ya pande zote nchini humo pamoja na jamii ya kimataifa.
-
Newsweek: Trump yumkini akafungwa jela miaka mitano
Feb 20, 2022 21:43Rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump, huenda akafungwa jela miaka mitano kwa madai kwamba alichukua nyaraka za siri za Ikulu ya Rais wa Marekani kuhusiana na usalama wa taifa alipoondoka madarakani mwaka jana.
-
Familia yalaani hukumu 'laini' dhidi ya polisi mzungu aliyeua kijana mweusi US
Feb 20, 2022 04:31Wanasheria na familia ya kijana mwenye asili ya Afrika aliyeuawa na polisi mzungu nchini Marekani mwaka jana wamelaani vikali kitendo cha kuhukumiwa kifungo cha miaka miwili pekee askari huyo muuaji katika mji Minneapolis.
-
Russia yamfukuza Naibu Balozi wa Marekani mjini Moscow
Feb 17, 2022 23:37Russia imemtimua mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa Marekani nchini humo, wakati huu ambapo nchi mbili hizo zinaendelea kuzozana kuhusu madai ya Wamagharibi kuwa serikali ya Moscow ina azma ya kuivamia kijeshi Ukraine.
-
Putin asisitiza, Russia haina nia ya kuingia vitani na Ukraine
Feb 16, 2022 23:18Rais Vladimir Putin wa Rassia aliuambia mkutano wa waandishi wa habari siku ya Jumanne baada ya kukutana na Kansela wa Ujerumani, Olaf Scholz, huko Kremlin kwamba ametoa wito kwa nchi za Magharibi kujiepusha kupeleka silaha za kivita kwenye mipaka ya Russia na kwamba zinapaswa kusitisha upanuzi wa shirika la NATO upande wa Mashariki.
-
Taliban yatishia kuangalia upya sera za Afghanistan kwa Marekani
Feb 15, 2022 23:05Serikali ya Taliban nchini Afghansitan imetishia kuangalia upya misimamo na sera zake kwa Marekani, iwapo Washington itakataa kuachia mabilioni ya fedha za Waafghani ilizozuilia.
-
Hotuba ya Imran Khan kuhusu kuwa na matokeo hasi vita vya Marekani dhidi ya ugaidi
Feb 15, 2022 23:05Waziri Mkuu wa Pakistan Imran Khan amekosoa sera na utendaji wa Marekani nchini Afghanistan na kusisitizia ulazima wa Washington kubadilisha mtazamo wake kuhusiana na hatua zake za kijeshi nje ya nchi; na akasema kuwa, vita vya Marekani dhidi ya ugaidi vimekuwa na matokeo hasi na vimesababisha kuongezeka ugaidi duniani.