-
Meja Jenerali Salami: Adui hawezi kuvumilia kuona Iran inastawi
Feb 04, 2021 23:23Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema maadui wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wanahamaki na kushindwa kuvumilia hatua za maendeleo na ustawi zinazopigwa na taifa hili.
-
Waziri: Magaidi wa ndani ya Marekani ndilo tishio kubwa kwa usalama wetu
Feb 04, 2021 23:22Waziri wa Usalama wa Ndani wa Marekani amekiri kwamba kuna magaidi ndani ya nchi hiyo na kwamba, magaidi hao ni tishio kubwa sana kwa nchi hiyo.
-
Misafara 2 ya kijeshi ya Marekani yashambuliwa nchini Iraq
Feb 04, 2021 23:21Duru za kiusalama zimeripoti habari ya kushambuliwa misafara miwili ya kilojistiki ya jeshi vamizi la Marekani katikati na kusini mwa Iraq.
-
Rais Rouhani: Kwa mara nyingine tena, Iran imeipiga mweleka Marekani
Feb 04, 2021 09:25Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC ya kukataa pingamizi la Marekani kuhusu mashataka ya Tehran dhidi yake, ni ushindi mwingine kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Marekani pia yarefusha kwa miaka 5 mingine mkataba wa New START iliosaini na Russia
Feb 04, 2021 00:56Baada ya muda wa chini ya wiki moja tangu rais wa Russia aliposaini mpango wa kurefusha mkataba wa New START, waziri wa mambo ya nje wa Marekani ametangaza kuwa nchi hiyo nayo pia imesaini mpango wa kurefusha mkataba huo.
-
Zarif: Marekani sharti itekeleze wajibu wake kwa kurejea katika JCPOA
Feb 02, 2021 00:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Marekani haina budi kutekeleza wajibu na majukumu yake kwa kurejea katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Blinken na madai mapya kwa ajili ya kurejea katika JCPOA
Feb 01, 2021 23:31Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani kwa mara nyingine tena amekariri hamu ya Washington ya kutaka kurejea katika mapatano ya JCPOA na kisha akatoa madai mapya kama sharti la kurejea katika mapatano hayo.
-
Marekani yaingiza shehena ya zana za kijeshi mashariki mwa Syria
Feb 01, 2021 23:30Duru mbalimbali za habari zimearifu kuwa, silaha na zana za kilojistiki za wanajaeshi magaidi wa Marekani zimeonekana zikiingizwa katika maidani ya mafuta huko Koniko kaskazini mashariki mwa Deir Zor.
-
Biden: Mamilioni ya watu wamepoteza ajira Marekani kutokana na corona
Feb 01, 2021 04:49Rais wa Marekani, Joe Biden amesema kuwa, mamilioni ya wananchi wa nchi hiyo hawana ajira baada ya kupoteza kazi zao kutokana na janga la ugonjwa wa COVID-19.
-
Kuchaguliwa Robert Malley kama mjumbe maalumu wa Marekani katika masuala ya Iran na kelele zisizo na maana zilizofuata
Jan 31, 2021 06:41Baada ya kuingia madarakani serikali mpya ya Joe Biden nchini Marekani na kutangazwa msimamo wake kuhusu mapatano ya nyuklia ya Iran ambayo ni maarufu kama JCPOA, ilikuwa inatarajiwa kuwa kungekuwa na mabadiliko maalumu katika uga huu.