-
Kuendelea vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran katika kivuli cha Corona
Mar 27, 2020 03:28Katika radiamali yake dhidi ya msimamo wa hivi karibuni wa Mike Pompeo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani juu ya kuendelea mashinikizo ya juu zaidi ya Washington dhidi ya Tehran, Muhammad Jawad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemtaja waziri huyo wa Marekani kuwa 'waziri wa chuki'.
-
Zarif: Janga la corona halisazi taifa lolote, hata Marekani inaomba msaada
Mar 26, 2020 22:33Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameiasi Marekani kubadili mienendo yake ili mripuko wa ugonjwa wa covid-19 ambalo ni janga la kimataifa lisilochagua taifa, usigeuke na kuwa mgogoro wa daima.
-
Waziri Zarif: Pompeo ni Waziri wa Chuki wa Marekani
Mar 26, 2020 06:38Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikali mienendo ya mwenzake wa Marekani, Mike Pompeo ya kueneza chuki, uhasama na propaganda dhidi ya Iran na kumtaja waziri huyo wa utawala wa Donald Trump kama Waziri wa Chuki.
-
Hitilafu za kisiasa zaongezeka nchini Marekani kuhusu makabiliano na Corona
Mar 26, 2020 00:58Kuenea virusi vya Corona na ugonjwa wa Covid-19 nchini Marekani si tu kwamba kumekuwa na taathira kubwa za kiuchumi na kijamii, bali pia kumegeuka na kuwa mjadala mkubwa ndani ya Bunge la Kongresi na ikulu ya White House.
-
Madai ya Pompeo: China na Russia zinaficha taarifa za virusi vya Corona
Mar 25, 2020 23:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amedai kuwa serikali za Russia na China zinajiepusha kutoa taarifa sahihi za virusi vya Corona.
-
Mwito wa wabunge wa Marekani wa kupunguzwa vikwazo vya nchi hiyo dhidi ya Iran
Mar 25, 2020 02:31Baada ya serikai ya Trump huko Marekani kujitoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei 2018, ilianza kuiwekea Iran vikwazo vya kila namna ambavyo Trump anajingamba kuwa hakuna nchi yoyote duniani iliyowahi kuwekewa vikwazo vikubwa, vikali na vingi kama alivyoiwekea Iran.
-
Shamkhani: Watawala wa Marekani wanatumia corona kama fursa ya kuendeleza uhasama
Mar 24, 2020 22:00Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesisitiza kuwa: "Watawala wa Marekani wanatumia corona kama fursa ya kuendeleza uhasama."
-
Kuna uwezekano watu milioni saba watafariki dunia nchini Marekani kutokana na corona
Mar 24, 2020 10:19Utafiti mpya uliofanywa hivi karibuni nchini Marekani umeonyesha kuwa, kutokana na uhaba wa vifaa vya kupumulia, watu zaidi ya milioni saba watafariki dunia endapo wataambukizwa kirusi cha corona.
-
Trump awataka Wamarekani wafungue biashara zao licha ya corona kuendelea kuua
Mar 24, 2020 03:01Rais wa Marekani, Donald Trump amewataka wananchi wa nchi hiyo kurejea katika biashara na shughuli zao za kila siku haraka iwezekanavyo akidai kuwa, idadi ya watu watakaojiua kutokana na msongo wa mawazo nchini humo itakuwa kubwa ikilinganishwa na ile ya wanaokufa kutokana na ugonjwa wa covid-19 (corona).
-
Viongoza wa New York waonya juu ya maafa yanayotokana na uhaba wa vifaa vya tiba
Mar 23, 2020 22:06Meya wa mji wa New York nchini Marekani ametahadharisha kuhusu ongezeko la hasara inayotokana na uhaba wa vifaa vya tiba na ametabiri kwamba, katika kipindi cha miezi miwili ijayo mgogoro unaotokana na virusi vya corona utakuwa mkubwa zaidi.