-
Vikwazo vipya vya Marekani na waitifaki wake wa eneo dhidi ya Iran na makundi ya muqawama
Oct 31, 2019 21:40Sera za serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani ni kuendelea kushadidisha mashinikizo dhidi ya Iran katika fremu ya 'mashinikizo ya juu kabisa' kwa kushirikiana na waitifaki wake. Kwa msingi huo Trump sasa anajaribu pia kuyawekea vikwazo makundi ya muqawama au mapambano ya Kiislamu katika eneo.
-
HRW: Askari wa Afghanistan waliopewa mafunzo na CIA wanafanya jinai za kivita
Oct 31, 2019 08:01Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limeripoti kuwa, kikosi cha askari wa Afghanistan kilichopewa mafunzo na kufadhiliwa na shirika la ujasusi la Marekani CIA kimefanya uhalifu wa kivita kutokana na mbinu zao za kuvamia makazi ya raia nyakati za usiku, kupoteza watu, kushambulia vituo vya afya na kuua raia.
-
Ukosoaji mkali wa Human Rights Watch kwa Marekani kutokana na vikwazo vyake dhidi ya Iran
Oct 30, 2019 10:10Baada ya kujitoa katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei 2018 serikali ya Donald Trump ya Marekani iliirejeshea Iran vikwazo vyote vilivyokuwa vimeondolewa baada ya mapatano hayo bali hata iliongeza vikwazo vingine vingi na kujigamba kuwa imeiwekea Iran vikwazo vya kiwango cha juu kabisa ambavyo havijawahi kuwekewa nchi yoyote ile duniani.
-
Marekani na magendo ya mafuta ya Syria
Oct 30, 2019 04:12Jumatatu iliyopita Mark Esper, Waziri wa Ulinzi wa Marekani alidai kuwa eti nchi yake ipo nchini Syria kwa ajili ya kulinda vyanzo vya mafuta vya taifa hilo la Kiarabu, na kwamba Washington haitaki kuona vyanzo hivyo vikiingia kwa mara nyingine katika udhibiti wa kundi la Daesh (ISIS).
-
Trump adai pia habari ya kuuawa mrithi wa Abubakar al-Baghdadi
Oct 30, 2019 01:07Rais Donald Trump wa Marekani ameandika katika mtandao wa kijamii wa Twitter kwamba askari wa Kimarekani wamemuua pia mrithi wa Abubakar al-Baghdadi, kiongozi wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS).
-
Marekani yadai imeitupa baharini maiti ya Abu Bakr al Baghdadi
Oct 29, 2019 13:06Mkuu wa majeshi ya Marekani amedai kuwa mwili wa aliyekuwa kiongozi wa kundi la kigaidi la Daesh, Abu Bakr al Baghdadi umetupwa bahaini baada ya kuthibitishwa kuwa wake kupitia kipimo cha vinasaba (DNA).
-
Mhimili wa Muqawama; ushindi katika medani ya vita dhidi ya maadui Asia Magharibi
Oct 29, 2019 08:14Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, mhimili wa muqawama katika eneo la Asia Magharibi ndiyo sababu ya kushindwa maadui na hivyo kuwafanya waanze kufanya njama dhidi ya harakati ya muqawama na eneo hili la Asia Magharibi.
-
Mshauri wa Spika wa Bunge: Kinara wa genge la kigaidi la DAESH alikuwa kikaragosi cha Marekani
Oct 28, 2019 04:05Mkurugenzi Mkuu wa masuala ya kimataifa wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema, kinara wa genge la kigaidi la DAESH (ISIS) Abubakar al-Baghdadi ni kikaragosi kilichotengezwa na Marekani ambacho muda wa matumizi yake ulikuwa umeshamalizika.
-
Kuangamizwa al Baghdadi na njama za Marekani za kujifanya inapambana na Daesh
Oct 28, 2019 02:29Marekani pamoja na waitifaki wake wa Kiarabu na Kimagharibi ndio waliolianzisha, kulitia nguvu na kuliunga mkono kwa kila namna na hali na mali; genge la kigaidi na la ukufurishaji la Daesh (ISIS) kwa shabaha ya kuiangusha serikali halali ya Syria.
-
Zarif amlaumu Trump kwa uongo wake mpya katika kushadidisha ugaidi wa kiuchumi dhidi ya wananchi wa Iran
Oct 27, 2019 23:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amemkosoa vikali rais wa Marekani, Donald Trump kwa uongo wake mpya katika kushadidisha ugaidi wa kiuchumi dhidi ya wananchi wa kawaida wa Iran.