-
Mkutano wa BRICS na tahadhari ya Putin kuhusu vikwazo vya Marekani
Nov 15, 2019 03:08Viongozi wa nchi wanachama katika jumuiya ya BRICS unayojumuisha nchi tano za Russia, Brazil, China, India na Afrika Kusini wamekutana katika mji mkuu wa Brazil, Brasilia. Mkutano huo umefanyika katika siku za tarehe 13 na 14 na ulilenga kupanua zaidi ushirikiano wa masuala ya kifedha na kiuchuni baina ya nchi wanachama na kuleta mabadiliko katika muundo wa sasa wa kimataifa.
-
Korea Kaskazini: Marekani na Korea Kusini zikifanya maneva ya kijeshi tutajibu
Nov 14, 2019 03:55Serikali ya Korea Kaskazini imetoa onyo jipya kwa viongozi wa Marekani kwamba, iwapo nchi hiyo kwa kushirikiana na Korea Kusini zitafanya maneva ya kijeshi, basi Pyongyang itajibu hatua hizo za uhasama.
-
UN yaitaka US iiondolee Iran vikwazo kama ilivyoagizwa na ICJ
Nov 13, 2019 23:13Umoja wa Mataifa umeitaka Marekani iheshimu agizo la Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu la kuiondolea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vikwazo vinavyohusiana na bidhaa za kibinadamu.
-
Rais wa Iraq ajibu uingiliaji wa Marekani katika masuala ya nchi hiyo
Nov 12, 2019 09:07Rais wa Iraq ametoa radiamali yake kwa taarifa ya uingiliaji ya Marekani kwa kusema: Mageuzi yanayotarajiwa huko Iraq kamwe hayapasi kuathiriwa na maamuzi kutoka nje.
-
Waziri Mkuu wa Sudan afanya mashauriano ili kuinasua nchi hiyo na vikwazo vya Marekani
Nov 12, 2019 08:40Waziri Mkuu wa Sudan amelazimika kuukimbilia Umoja wa Ulaya katika juhudi za kuupatia ufumbuzi mgogoro wa kisiasa na kiuchumi wa nchi yake uliosababishwa na vikwazo vya Marekani.
-
Araqchi: Iran imepunguza uwajibikaji wake ili kuyalinda makubaliano ya JCPOA
Nov 12, 2019 08:34Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran katika Masuala ya Kisiasa amesema kuwa lengo la Tehran kupunguza ahadi na uwajibikaji wake katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ni kwa ajili ya kuyalinda makubaliano hayo.
-
"Marekani inachochea maandamano katika nchi za Kiarabu kwa maslahi yake"
Nov 12, 2019 04:41Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, Marekani inatumia maandamano yanayoshuhidiwa hivi sasa katika nchi kadhaa za Kiarabu kusukuma ajenda zake, na kuifanya Lebanon ishindwe kujisimamia yenyewe.
-
Indhari ya Mshauri wa Usalama wa Taifa Marekani kuhusu kusambaratika NATO
Nov 12, 2019 04:27Rais Donald Trump wa Marekani ambaye ni maarufu kwa kuibua utata, angali anaendelea kukosoa vikali Muungano wa Kijeshi wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) . Trump hasa anawakosoa wanachama wa bara Ulaya katika muungano huo kwa kutotenga asilimia 2 ya Pato la Ndani la Nchi (GDP) kwa ajili ya gharama za kijeshi. Maafisa wa ngazi za juu wa Marekani nao sasa pia wanafuata nyayo za Trump katika kuukosoa muungano wa kijeshi wa NATO.
-
Sisitizo la jeshi la Marekani la kuendelea kuwepo kijeshi katika eneo la Asia Magharibi
Nov 11, 2019 23:26Licha ya Rais Donald Trump kukariri mara chungu nzima kwamba, Washington itaondoa wanajeshi wake katika eneo la Asia Magharibi hususan katika nchi za Syria na Afghnaistan, lakini hali ya mambo ilivyo inaonyesha kuwa, Marekani imeazimia kubakisha na hata kuongeza idadi ya wanajeshi wake pamoja na zana za kijeshi katika eneo hili ikiwa ni katika kusukuma mbele gurudumu la siasa zake za kibabe.
-
Uturuki yamrejesha mwanachama wa ISIS nchini Marekani
Nov 11, 2019 07:54Uturuki imesema imemrejesha mwanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) katika nchi yake ya Marekani, huku Ankara ikianza kuwarejesha makwao magaidi wa genge hilo la ukufurishaji iliowakamata.