-
Mgombea wa uchaguzi wa rais Marekani atiwa nguvuni katika maandamano ya watetezi wa Palestina
Apr 28, 2024 23:06Polisi nchini Marekani imemtia nguvuni mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi wa mwaka huu nchini humo ambaye alikuwa katika maandamano ya kuiunga mkono Palestina yaliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Washington.
-
Intelijinsia Marekani: Putin hakuamuru kuuliwa Navalny
Apr 28, 2024 23:06Jarida la Wall Street limezinukuu duru za kiintelijinsia za Marekani na kuripoti kuwa Rais Vladmir Putin wa Russia hakuagiza kuuawa mwanasiasa wa upinzani wa nchi hiyo, Alexei Navalny, aliyefia gerezani mwezi Februari mwaka huu.
-
Wachambuzi: Maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu Marekani yanamuweka Biden matatani
Apr 27, 2024 08:14Duara la maandamano ya wanafunzi wa vyuo viku dhidi ya vita vya Israel katika Ukanda wa Gaza linazidi kupanuka nchini Marekani, na kusababisha mkanganyiko mkubwa katika hesabu za Israel na waungaji mkono wake.
-
Ukosoaji wa Amnesty International kwa njama za Marekani za kuficha jinai za Israel Gaza
Apr 26, 2024 23:05Agnes Callamard, Katibu Mkuu wa Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International, ameonya kuhusu kuendelea kwa ukiukaji wa haki za binadamu huko Gaza na kutangaza kuwa: Marekani inazuia kutuhumiwa Israel kwa kukiuka haki za binadamu katika Ukanda wa Gaza.
-
Marekani yashadidisha ukandamizaji dhidi ya wapinzani wa utawala wa Kizayuni na waungaji mkono wa Palestina
Apr 25, 2024 23:39Marekani ndiyo muungaji mkono mkubwa zaidi wa utawala wa Kizayuni wa Israel ambapo serikali ya Biden imetoa msaada mkubwa zaidi wa kijeshi na silaha kwa Tel Aviv wakati wa vita vya Gaza, ambavyo vimeingia katika mwezi wake wa saba.
-
Spika wa zamani wa Marekani: Netanyahu anapaswa ajiuzulu, amekwamisha amani kwa miaka kadhaa
Apr 25, 2024 06:31Spika wa zamani wa Baraza la Wawakilishi la Marekani Nancy Pelosi amesema, waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel ni kizuizi cha kupatikana amani Ghaza na anapaswa ajiuzulu.
-
Kan'ani: Ukiukaji wa haki za binadamu nchini Marekani umeitia wasiwasi dunia
Apr 24, 2024 08:41Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, ukiukaji wa kutisha wa haki ya kupiga kura, uhuru wa kusema na haki za binadamu huko Marekani unawatia wasiwasi mkubwa watu duniani.
-
Msemaji wa Serikali ya Iran: Kuna Pengo kubwa kati ya viongozi wa Marekani na maoni ya umma
Apr 24, 2024 02:55Msemaji wa Serikali ya Iran amesema, akizungumzia msaada mpya wa kifedha wa Marekani kwa utawala wa Kizayuni wa Israel, kwamba: Pengo kubwa lililopo kati ya watawala walioathiriwa na Uzayuni na maoni ya umma katika nchi za Magharibi haliwezi kukanushwa tena.
-
Kushindwa njama za Marekani za kutaka kuendelea kuwa na uwepo wa kijeshi nchini Niger
Apr 23, 2024 23:02Baada ya kugonga mwamba mazungumzo ya kisiasa ya Marekani ya kudumisha uwepo wake wa kijeshi nchini Niger, kwa mara nyingine tena raia katika nchi hiyo ya Kiafrika wametoa mwito wa kuondoka kwa wanajeshi wa Marekani katika nchi yao kwa kufanya maandamano mbele ya kambi ya kijeshi ya Marekani kaskazini mwa Niger.
-
Waandishi wakosoaji wa Israel wasusia tamasha la jumuiya ya PEN America
Apr 23, 2024 06:54Tamasha ya Jumuiya ya Kalamu ya Marekani (PEN America) imefutwa kutokana na ukosoaji mkubwa wa waandishib walioalikwa katika sherehe hiyo dhidi ya jinai na uhalifu unaofanywa na Israel huko Gaza.