-
Kamanda Salami: Vita vya Gaza vimeifedhehesha Marekani
Mar 08, 2024 03:53Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) amesema mauaji ya wanawake, watoto wadogo na raia wengine wasio na hatia katika Ukanda wa Gaza si kitu chochote kingine ghairi ya aibu na fedheha kwa Marekani.
-
Marekani yafanya kimya kimya mauzo 100 ya silaha kwa Israel
Mar 08, 2024 00:10Ripoti mpya imefichua kuwa, Marekani imeidhinisha kimya kimya mauzo 100 ya silaha kwa Israel tangu utawala huo wa Kizayuni uanzishe vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza Oktoba 7, 2023.
-
Ukosoaji wa UN wa mashambulizi ya makusudi ya Israel dhidi ya misafara ya misaada huko Gaza
Mar 06, 2024 08:01Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki ya Chakula ametangaza kwamba, jeshi la Israel linashambulia kwa makusudi misafara ya misaada ya kibinadamu huko Gaza licha ya kujua njia za misafara hiyo.
-
Kuongezeka uungaji mkono wa wananchi wa Marekani kwa Wapalestina
Mar 05, 2024 04:12Matokeo ya uchunguzi wa maaoni uliofanywa na jarida la Wall Street Journal yanaonyesha kuwa, wananchi wengi wa Marekani hawaridhishwi na utendaji kazi wa Rais Joe Biden katika vita vya Gaza.
-
Kuongezeka mgawanyiko katika Baraza la Mawaziri la Vita la utawala wa Kizayuni kutokana na safari ya Gantz nchini Marekani
Mar 03, 2024 22:58Safari ya Benny Gantz, mmoja wa wajumbe wa Baraza la Mawaziri la Vita la utawala wa Kizayuni huko Marekani imekosolewa vikali na Benyamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala huo.
-
Mamia waandamana nje ya ubalozi wa Israel, Washington kulaani vita Gaza
Mar 03, 2024 04:10Mamia ya watu wamefanya maandamano mbele ya ubalozi wa Israel mjini Washington, Marekani kulaani vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Ushiriki wa Wairani katika uchaguzi, jibu kwa misimamo ya uingiliaji kati hasi ya Merekani
Mar 02, 2024 10:11Kushiriki kwa wananchi wa Iran katika uchaguzi wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge) na Baraza la Wataalamu Wamaomchagua Kiongozi Mkuu, kwa mara nyingine tena, kumezima njama za wapinzani wa Jamhuri ya Kiislamu wakiongozwa na Marekani, za kuwakatisha tamaa wananchi ili wasishiriki katika upigaji kura.
-
Wosia wa Bushnell: Majivu ya mabaki yangu yamiminwe Palestina
Mar 02, 2024 08:19Aaron Bushnell, afisa wa Jeshi la Anga la Marekani, ambaye alifariki dunia hivi karibuni baada ya kujichoma moto akipinga uungaji mkono wa nchi yake kwa vita vya mauaji ya kimbari vya utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza, aliandika katika wosia wake kuwa majivu ya mabaki ya mwili wake yamiminwe katika ardhi ya taifa huru la Palestina.
-
Iran yaionya UN: Marekani inashadidisha taharuki katika eneo
Feb 27, 2024 03:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikali juhudi za Marekani za kushadidisha hali ya taharuki katika Bahari Nyekundu na Yemen na kuonya kuwa, hatua hizo za kijeshi za Washington hazitakuwa na matokeo mengine isipokuwa kuvuruga jitihada za pamoja za Iran na Umoja wa Mataifa katika eneo la Asia Magharibi.
-
Waziri wa Ulinzi wa Yemen: Zama za Marekani na waitifaki wake 'kuhodhi' maji ya kimataifa zimekwisha
Feb 26, 2024 07:58Waziri wa Ulinzi wa Yemen amepongeza operesheni za majini zinazoendelea kufanywa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya meli zenye uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Bahari Nyekundu kwa lengo la kupinga vita dhidi ya Ghazza, na kusisitiza kwamba zama za "satua ya kuhodhi" Marekani na washirika wake maji ya kimataifa zimekwisha.