-
Kan'ani: Marekani na Uingereza zinatoa kafara usalama wa kimataifa kwa maslahi ya Israel
Feb 25, 2024 23:32Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Iran amelaani vikali mashambulizi mapya ya anga ya "kiholela" yaliyofanywa na Marekani na Uingereza dhidi ya Yemen, akisema hujuma hiyo imethibitisha kwa mara nyingine kwamba nchi hizo mbili zinatoa kafara usalama wa kimataifa kwa maslahi ya Israel.
-
Trump: Hali mbaya zaidi inaisubiri Marekani iwapo Biden atashinda 2024
Feb 25, 2024 06:53Donald Trump, rais wa zamani wa Marekani kwa mara nyingine amemshambulia Rais wa sasa wa nchi hiyo Joe Biden akisisitiza kuwa, Wamarekani watakabiliwa na hali mbaya zaidi iwapo Biden atashinda muhula wa pili katika uchaguzi wa rais wa mwaka huu.
-
Sudan yapuuzilia mbali madai ya Marekani dhidi yake
Feb 25, 2024 06:26Serikali ya Sudan imekosoa vikali taarifa ya Marekani inayotuhumu serikali ya Khartoum kwamba inazuia watu nchi humo kufikishiwa misaada ya kibinadamu.
-
HAMAS: Kimbunga cha al-Aqsa kimevuruga njama za US katika eneo
Feb 23, 2024 00:00Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa iliyofanywa na makundi ya muqawama ya Ukanda wa Gaza ilisitisha njama za Marekani za eti kulifinyanga eneo la Asia Magharibi na mustakabali wake.
-
Walimwengu wailaani US kwa kutumia veto kuzuia usitishaji vita Gaza
Feb 20, 2024 23:27Mataifa na mashirika mbali mbali ya kimataifa yamelaani vikali hatua ya Marekani ya kutumia kura yake ya turufu kupinga rasimu ya azimio iliyowasilishwa na Algeria katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, la kutaka kusitishwa mara moja mapigano katika Ukanda wa Gaza.
-
Iran: Kuipatia Israel dola bilioni 14 ni sawa na Marekani kutoa bakhshishi kwa mauaji ya Wapalestina
Feb 19, 2024 07:45Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema, kuidhinishwa na Baraza la Seneti la Marekani msaada wa dola bilioni 14 kwa utawala wa Kizayuni wa Israel kunaonyesha kuwa Washington inautuza na kuupa bakhshishi utawala huo kwa kuwaua kwa halaiki raia wasio na hatia wa Palestina katika vita visivyo na mlingano vya Gaza.
-
Yemen: Tumeitwanga meli ya Uingereza na kuitungua ndege isiyo na rubani ya Marekani
Feb 19, 2024 07:36Msemaji wa vikosi vya ulinzi vya Yemen ametangaza kuwa, katika kuonyesha mshikamano na uungaji mkono kwa taifa la Palestina na kujibu mashambulio na uchokozi wa Marekani na Uingereza dhidi ya ardhi ya Yemen, vikosi vya nchi hiyo vimeipiga makombora kadhaa meli ya Uingereza katika operesheni maalumu viliyotekeleza katika Ghuba ya Aden.
-
US kuipigia veto rasimu ya azimio la Algeria la kusitisha vita Gaza
Feb 18, 2024 07:35Maafisa wa Marekani wameapa kuwa nchi hiyo itatumia kura yake ya turufu kupinga rasimu ya azimio iliyowasilishwa na Algeria katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, la kutaka kusitishwa mara moja mapigano katika Ukanda wa Gaza.
-
Biden aambiwa: Sitisha vita Gaza iwapo unataka kura za Waislamu
Feb 18, 2024 07:35Meya wa jiji la Dearborn, kaunti ya Wayne katika jimbo la Michigan nchini Marekani amesema Rais Joe Biden wa hiyo hatapata kura za Waislamu katika uchaguzi ujao nchini humo, iwapo ataendelea kuunga mkono jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni katika vita vya Gaza.
-
Marekani kuitumia Israel mamia ya mabomu aina ya MK-82
Feb 17, 2024 08:04Serikali ya Rais Joe Biden wa Marekani inapanga kutuma shehena za mabomu na silaha nyingine zenye thamani ya makumi ya mamilioni ya dola kwa utawala wa Kizayuni wa Israel unaoendelea kumwaga damu za Wapalestina wasio na hatia katika Ukanda wa Gaza.