-
Iran: Wanyonyaji damu wa Kizayuni wameanzisha upya mauaji Gaza kwa uungaji mkono wa US
Dec 01, 2023 07:35Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: baada ya kuwaua zaidi ya Wapalestina 15,000, wanyonyaji damu wa Kizayuni wameanzisha duru mpya ya mauaji huko Gaza kwa uungaji mkono kamili wanaoendelea kupewa na serikali ya Marekani.
-
Onyo la Moscow kuhusu kuendelea vita vya Ukraine mwaka 2024
Dec 01, 2023 04:29Licha ya kupita karibu miezi 22 tangu kuanza vita vya umwagaji damu nchini Ukraine, lakini hakuna matumaini yoyote yanayoashiria kumalizika mzozo huo hivi karibuni. Hii ni katika hali ambayo nchi za Magharibi kwa sasa zimeshughulishwa na vita vya Gaza na hivyo kutozingatia sana vita vya Ukraine, jambo ambalo limeipelekea serikali yenye mielekeo ya Kimagharibi ya Kyiv kukata tamaa kuhusu kupata misaada zaidi ya nchi hizo.
-
Russia yailaumu Marekani kwa mgogoro wa Gaza
Nov 30, 2023 00:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia amesema Marekani inapasa kubebeshwa dhima ya mgogoro baina ya Palestina na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Iran yazionya Marekani na Israel juu ya 'matokeo hasi makali' endapo jinai za kivita zitaendelea Gaza
Nov 28, 2023 09:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian amezionya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwamba zitakabiliwa na "matokeo hasi makali" iwapo zitashindwa kukomesha kikamilifu uhalifu wa kivita katika Ukanda wa Gaza uliofanywa wakati wa vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya eneo Palestina lililowekewa mzingiro.
-
Jeshi la Iran: Manowari ya Kimarekani yakubaliwa kuingia Ghuba ya Uajemi baada ya kujibu maswali yote ya Wanamaji wa Iran
Nov 28, 2023 04:14Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC amesema: Meli ya kubeba ndege za kivita ya Marekani ilikubaliwa kuingia Ghuba ya Uajemi kupitia Lango Bahari la Hormuz baada ya kujibu maswali yote ya vikosi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa lugha ya kifarsi.
-
Jeshi la Yemen laivurumishia makombora manowari ya US
Nov 27, 2023 07:16Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani katika eneo la Asia Magharibi (CENTCOM) limetangaza habari ya vikosi vya Jeshi la Yemen kuvurumisha makombora mawili ya balestiki na kulenga meli ya kivita ya Marekani ya 'USS Mason' katika Ghuba ya Aden.
-
Kufukuzwa Manowari ya Marekani kutoka kwenye maji ya China
Nov 26, 2023 23:14Ingawa muda mrefu haujapita tangu kufanyika kikao kati ya marais wa Marekani na China mjini San Francisco, kikao ambacho Rais Joe Biden wa Marekani alikitaja kuwa chanya, Tian Junli, Msemaji wa Kamandi ya Pamoja ya Vikosi vitatu vya Jeshi la Nchi Kavu, Anga na Baharini vya Jeshi la China ametangaza kufukuzwa manowari ya Marekani kutoka kwenye eneo la maji ya nchi hiyo.
-
Harakati ya Fat'h ya Iraq: Vita dhidi ya Wazayuni ndio kwanza vimeanza
Nov 26, 2023 08:33Mjumbe wa Muungano wa al Fat'h wa Iraq ameashiria jinsi makundi ya muqawama ya nchi hiyo yanavyoyaunga mkono makundi ya muqawama ya Palestina katika vita vya Ghaza na kusema kuwa, makundi hayo yataendelea kushambulia vituo vya wanajeshi vamizi wa Marekani nchini Iraq.
-
Al-Khazali: Marekani haitaki kuondoka Iraq, inatumia kisingizio cha kupambana na Daesh
Nov 25, 2023 09:33Kiongozi wa harakati ya muqawama ya Iraq amesema kuwa, vikosi vya majeshi ya Marekani havina nia ya kuondoka katika nchi hiyo ya Kiarabu na vinahalalisha uwepo wao kinyume cha sheria kwa kutumia kisingizio cha kupambana na kundi la kigaidi la Daesh ambalo limekwishakufa na kutoweka.
-
Amir-Abdollahian: Uungaji mkono wa Marekani kwa Israel ulisababisha kuendelea kwa vita Gaza
Nov 24, 2023 08:32Waziri wa Mashauriano ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kama si msaada na himaya ya Marekani kwa utawala ghasibu wa Israel, utawala huo bandia haungeweza kuendeleza vita na Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS).