-
Marekani kukanusha tena kutokea mauaji ya kimbari huko Ukanda wa Gaza, ni kukana ukweli ulio wazi
May 16, 2024 00:55Licha ya Wapalestina zaidi ya elfu 35,000 kuuawa shahidi na utawala wa kigaidi wa Israel huko Ukanda wa Gaza, lakini Jake Sullivan, Mshauri wa Usalama wa Taifa wa Ikulu ya White House nchini Marekani amedai bila kuona haya kwamba serikali ya Rais Joe Biden haiyachukulii mauaji hayo kuwa ni mauaji ya halaiki.
-
Magharibi iliiomba Iran 'isiipige sana Israel', ipunguze ukali wa operesheni ya Ahadi ya Kweli
May 09, 2024 00:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema nchi za Magharibi ziliiomba Jamhuri ya Kiislamu ijizuie na ipunguze ukali wa operesheni yake ya kulipiza kisasi dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel, kabla ya kushambulia vituo vya utawala huo mwezi uliopita kujibu mapigo kwa shambulio lake la kigaidi ulilofanya dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran nchini Syria.
-
Mauaji ya kimbari Ukanda wa Gaza na uwezekano wa Qatar kuangalia upya sera zake za kigeni za usuluhishi
Apr 20, 2024 22:47Muhammad bin Abdulrahman Al Thani Waziri Mkuu wa Qatar amesema kuwa nchi hiyo inatathmini upya nafasi yake kama msuluhishi kati ya Israel na Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas).
-
Mwakilishi wa Iran UN: Marekani imetumia unafasi yake kuunga mkono mauaji ya kimbari huko Gaza
Apr 09, 2024 08:41Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, Marekani imetumia sifa na nafasi yake kuunga mkono mauaji ya kimbari ya utawala wa Kizayuni wa Israel huko Gaza.
-
Sababu za utawala wa Kizayuni kulazimisha vita katika upande wa kaskazini
Apr 01, 2024 22:49Yoav Gallant, Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni, amesema kwamba utawala huo haramu utapanua operesheni zake za kijeshi katika eneo la kaskazini la ardhi zinazokaliwa kwa mabvu na kushambulia kila sehemu ya Beirut na Damascus ambapo Hizbullah ya Lebanon inaendeshea shughuli zake.
-
Corbyn: Kuendelea Uingereza kuipa Israel silaha kunaifanya mshirika katika mauaji ya kimbari Gaza
Apr 01, 2024 07:14Kiongozi wa zamani wa chama cha Labour nchini Uingereza amezikosoa nchi za Magharibi - hasa Marekani na Uingereza - zinazoendelea kuipatia Israel silaha za kuwaua Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, na kusema kuwa nchi hizo zinakiuka sheria za kimataifa.
-
Kupokewa vizuri ripoti ya UN kuhusu mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel huko Ghaza
Mar 28, 2024 23:08Tathmini ya ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya Palestina juu ya mauaji ya umati yanayofanywa na Israel kwenye Ukanda wa Ghaza imepokewa vizuri na kuungwa mkono na wawakilishi wa nchi za dunia ndani ya umoja huo.
-
Ulimwengu waunga mkono ripoti ya UN kuhusu mauaji ya kimbari ya Israel Ukanda wa Gaza
Mar 27, 2024 08:36Tathmini iliyofanywa na Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Masuala ya Palestina ambayo imezitaja jinai za utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Gaza kuwa ni mauaji ya kimbari imeungwa mkono pakubwa na nchi mbalimbali katika umoja huo.
-
Borrell: Israel inafanya mauaji ya halaiki dhidi ya watu wa Gaza
Mar 15, 2024 22:53Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya ambaye katika siku za hivi karibuni ameutuhumu utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa unatumia "njaa kama silaha" katika vita vya Gaza, ameonya kuwa utawala huo unawaua watu wa Gaza kwa umati.
-
Haniyeh awataka Wapalestina kuandamana kwenye Msikiti wa Al-Aqsa siku ya 1 ya Ramadhani
Feb 29, 2024 08:37Mkuu wa Ofisi ya Siasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amewataka Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu na Israel kuandamana hadi Msikiti wa Al-Aqsa katika siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.