-
Al Bashir: Eneo la Halayeb ni milki ya Sudan
Sep 30, 2018 10:38Rais wa Sudan amesema tena kwamba eneo linalogombaniwa la Halayeb ni milki ya nchi yake na kwamba Khartoum inazo nyaraka za kihistoria zinazothibitisha madai hayo.
-
Wanaharakati Misri watoa wito wa kukabiliana na kanali 27 za satalaiti za TV za Kiarabu zinazoanzishwa na Israel
Sep 27, 2018 12:17Wanaharakati nchini Misri wametaka zichukuliwe hatua kukabiliana na kampeni inayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuanzisha kanali za televisheni za satalaiti za lugha ya Kiarabu.
-
Mahkama ya Misri yakataa pendekezo la kufanya maridhiano na dikteta Mubarak
Sep 24, 2018 11:02Vyombo vya Mahkama nchini Misri vimetupilia mbali pendekezo la kuridhiana na dikteta aliyeuzuliwa madarakani Hosni Mubarak, pamoja na watoto wake.
-
Makumi ya wafuasi wa Ikhwanul Muslimin wafungwa maisha nchini Misri
Sep 23, 2018 11:14Kiongozi wa kundi la Ikhwanul Muslimin la Misri na makumi ya wananchama wa kundi hilo wamehukumiwa kifungo cha maisha jela nchini Misri.
-
Ukosoaji wa Amnesty International kwa ukatili na ukandamizaji unaofanywa na serikali ya Misri
Sep 19, 2018 22:09Wakati serikali ya Rais Abdel Fattah el-Sisi inaendelea kuwabana na kuwakandamiza wapinzani kwa kutoa hukumu za adhabu kali dhidi yao Shirika la Msamaha Duniani Amnesty International limeeleza kwamba ukandamizaji unaofanywa na serikali ya Cairo dhidi ya uhuru wa kutoa maoni tangu el-Sisi ashike hatamu za madaraka ya nchi ni wa "kiwango cha kutisha na haujawahi kushuhudiwa."
-
Amnesty International: Ukandamiza wa uhuru wa kujieleza Misri umevuka mpaka
Sep 18, 2018 22:40Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetangaza kuwa, ukandamizaji wa uhuru wa kujieleza nchini Misri katika kipindi hiki cha utawala wa Abdel Fattah al Sisi umefikia kiwango cha tahadhari na haujawahi kuonekana nchini humo.
-
Wafungwa wa kisiasa wanakabiliwa na hali mbaya katika jela za Misri
Sep 13, 2018 09:15Hali ya wafungwa wa kisiasa nchini Misri miaka mitano baada ya mapinduzi ya kijeshi nchini humo inaripotiwa kuwa mbaya sana.
-
EU yalaani kuhukumiwa kifo wananchama wa Ikhwani, Misri
Sep 11, 2018 20:50Umoja wa Ulaya umelaani hukumu ya kifo iliyotolewa na mahakama moja nchini Misri, dhidi ya makumi ya wanachama wa harakati ya Ikhwanul Muslimin.
-
Wanachama 75 wa Ikhwanul Muslimin wahukumiwa kifo nchini Misri
Sep 08, 2018 21:51Mahakama ya rufaa ya Misri imewahukumu adhabu ya kifo wanachama 75 wa kundi la Ikhwanul Muslimin kwa tuhuma za kuhusika katika matukio yanayojulikana kwa jina la "Rābiʿa al-ʿAdawiyya" kama ambavyo pia imewahukumu kifungo cha maisha jela wanachama wengine 46 wa kundi hilo.
-
Rais Sisi aidhinisha sheria inayodhibiti matumizi ya mitandao
Sep 02, 2018 22:15Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi ameidhinisha sheria mpya ya kudhibiti mitandao ya kijamii katika kile kinachotajwa kuwa ni muendelezo wa sera za kukandamiza upinzani.