-
Magaidi 13 waangamizwa na polisi ya Misri Peninsula ya Sinai
Jul 26, 2018 02:01Jeshi la Polisi la Misri limetangaza habari ya kuua wanachama 13 wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) katika eneo la Sinai, kaskazini mwa nchi.
-
Kituo cha Fatwa Misri: Kuna ushahidi kwamba Israel inawasaidia magaidi wa Daesh
Jul 25, 2018 08:42Kituo cha fatwa nchini Misri kimetangaza kwamba, kuna ushahidi madhubuti kwamba utawala haramu wa Israel unalisaidia kundi la kigaidi la Daesh na makundi mengine ya Kiwahabi yanayohusika na machafuko nchini Syria.
-
Bunge la Misri lapasisha sheria inayowapa kinga majenerali wa jeshi
Jul 16, 2018 22:25Bunge la Misri Jumatatu ya jana lilipasisha sheria inayowapa kinga ya kufikishwa mahakamani majenerali wa jeshi wanaohusishwa na machafuko yaliyotokea baada ya mapinduzi ya Rais wa kwanza kuchaguliwa kwa njia za kidemokrasia nchini humo. Maelfu ya raia wa Misri walimiminika mitaani kupinga mapinduzi ya jeshi yaliyomuondoa madarakani Mohamed Mursi.
-
Jeshi la Misri laangamiza magaidi 11 Peninsula ya Sinai
Jul 11, 2018 09:03Jeshi la Misri limetangaza habari ya kuua wanachama 11 wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) katika eneo la Sinai, kaskazini mwa nchi.
-
Ikhwanul Muslimin wakanusha kufanya mazungumzo ya siri na serikali ya Misri
Jul 07, 2018 00:09Msemaji wa harakati ya Ikhwanul Muslimin ya Misri amekanusha habari ya kufanyika mazungumzo ya siri baina ya harakati hiyo kubwa zaidi ya kisiasa ya upinzani na serikali ya nchi hiyo.
-
Misri: Migogoro ya kieneo haiwezi kupatiwa ufumbuzi kwa mtutu wa bunduki
Jul 05, 2018 03:03Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Misri amesema kuwa, nchi yake inafanya juhudi kubwa katika mwenendo wa kupatiwa ufumbuzi migogoro wa Syria na Libya na kusisitiza kwamba, migogoro inayoshuhudiwa hivi sasa katika eneo la Mashariki ya Kati na kaskazini mwa Afrika ufumbuzi wake sio mtutu wa bunduki.
-
Ikwanul Muslimin yapinga hatua ya al Sisi ya kuwapa kinga makamanda wa jeshi la Misri
Jul 04, 2018 08:42Msemaji wa harakati ya Ikhwanul Muslimin nchini Misri amekosoa hatua ya serikali ya Jenerali Abdul Fattah al Sisi ya kuimarisha nafasi ya wanajeshi nchini humo na mwafaka wa Bunge wa kuwapa kinga ya sheria makamanda wa jeshi la nchi hiyo.
-
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yaitaka Ufaransa iache kuiuzia silaha Misri
Jul 02, 2018 03:13Mashirika kadhaa ya kutetea haki za binadamu yameitaka serikali ya Ufaransa kusimamisha uuzaji wa silaha kwa Misri, yakisisitiza kuwa silaha hizo zinatumiwa na vyombo vya usalama kuwanyamazisha na kuwawekea mbinyo wapinzani na wakosoaji wa serikali.
-
Makahama ya Misri yaakhirisha hukumu ya watuhumiwa wa Medani ya Rabia
Jun 30, 2018 11:46Mahakama ya Jinai ya Cairo leo Jumamosi imeamua kuakhirisha hukumu ya mwisho dhidi ya watu 739 walioshiriki katika maandamano ya mwaka 2013 ambayo yalisambaratishwa kwa mabavu na vyombo vya usalama na kusababisha moja kati ya mauaji makubwa zaidi ya raia katika historia ya sasa ya nchi hiyo.
-
"Saudia iliipa hongo timu ya taifa ya Misri ikubali kuifunga kombe la dunia" - Mwandishi
Jun 27, 2018 03:25Mwandishi mmoja wa Misri amelalamika kuwa serikali ya nchi yake ilipokea rushwa na hongo kutoka kwa Saudi Arabia na kuilazimisha timu ya taifa ya nchi hiyo ikubali kufungwa na Saudia katika mashindano ya fainali za kombe la dunia yanayoendelea nchini Russia hivi sasa.