-
Zaidi ya wanafunzi 200 waliokuwa wametekwa nyara Nigeria wameachiwa huru
Mar 24, 2024 03:33Zaidi ya wanafunzi 200 pamoja na wafanyakazi waliokuwa wametekwa nyara na watu wenye silaha katika skuli moja kaskazini mwa Nigeria mapema mwezi huu wameachiliwa. Hayo ni kwa mujibu wa ofisi ya gavana wa jimbo la Kaduna lililoko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
-
Wahalifu wenye silaha wawateka nyara watu zaidi ya 100 huko Nigeria
Mar 19, 2024 08:19Wahalifu wenye silaha wamewateka nyara zaidi ya watu 100 katika mashambulizi mawili mapya kaskazini magharibi mwa Nigeria, ikiwa zimepita wiki kadhaa baada ya wanafunzi 250 wa shule kutekwa nyara nchini humo.
-
Rais wa Nigeria aliagiza jeshi liwasake walioua askari 16 Delta
Mar 18, 2024 23:08Rais wa Nigeria Bola Ahmed Tinubu ameliamrisha jeshi la nchi hiyo kuwasaka na kuwafikisha katika vyombo vya dola wahusika wa mauaji ya wanajeshi 16 wa nchi hiyo katika jimbo la kusini la Delta.
-
Visa zaidi vya utekaji nyara vyahofiwa Nigeria
Mar 11, 2024 22:45Serikali ya Shirikisho ya Nigeria imeorodhesha shule kadhaa katika majimbo 14 nchini humo kuwa ni maeneo yaliyoko hatarini kushambuliwa na majambazi na wahalifu wenye silaha.
-
Rais wa Nigeria alituma jeshi kwenda kuokoa wanafunzi zaidi ya 250 waliotekwa nyara
Mar 09, 2024 04:12Rais Bola Ahmed Tinubu wa Nigeria ametuma wanajeshi kwenda kuwaokoa zaidi ya wanafunzi 250 waliotekwa nyara na watu wenye silaha kutoka shule moja kaskazini magharibi mwa nchi hiyo katika mojawapo ya matukio makubwa zaidi ya utekaji nyara kushuhudiwa katika kipindi cha miaka mitatu.
-
Nigeria yasema itaomba kujiunga na jumuiya ya kiuchumi ya BRICS
Mar 08, 2024 06:38Waziri wa Mambo ya Nje wa Nigeria Yusuf Tuggar amesema nchi yake inajipanga kuomba uanachama katika jumuiya ya kiuchumi ya BRICS baada ya mipango muhimu ya uratibu wa ndani ya nchi hiyo kukamilika.
-
Wabeba silaha wavamia shule na kuteka nyara watoto 225 Nigeria
Mar 08, 2024 03:53Watu wenye silaha wameshambulia shule na kuwateka nyara watoto zaidi ya 200 huko kaskazini magharibi mwa Nigeria.
-
Waziri wa Nigeria: Mauaji ya Wapalestina Gaza hayahalalishiki
Mar 06, 2024 08:14Waziri wa Mambo ya Nje wa Nigeria amesema vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza haviwezi kuhalalalishika kwa njia yoyote ile.
-
Nigeria: Mwezi huu tutatoa ripoti kuhusu mashambulizi ya anga yaliyouwa raia
Feb 21, 2024 07:57Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Jeshi la Nigeria, Jenerali Christopher Musa, amesema kuwa ripoti kuhusu mashambulizi ya anga ya ndege zisizo na rubani (droni) yaliyouwa raia karibu 85 katika jimbo la Kaduna kaskazini mwa nchi Disemba mwaka jana zitatolewa mwishoni mwa mwezi huu.
-
Watu 4 wauawa, 40 watekwa nyara kaskazini mwa Nigeria
Feb 14, 2024 04:04Kwa wakali watu wanne wameuawa huku makumi ya wengine wakitekwa nyara katika shambulio lililofanywa na kundi moja la wabeba silaha katika jimbo la Zamfara la kaskazini magharibi mwa Nigeria.