-
Rais Buhari wa Nigeria aongeza muda wa kubadilisha noti za zamani hadi Aprili
Feb 17, 2023 10:12Rais wa Nigeria, Muhammadu Buhari, ametoa idhini kwa Benki Kuu ya nchi hiyo kuongeza muda wa mwisho wa kubadilisha noti za zamani za pesa za nchi hiyo hadi Aprili 10 mwaka huu, baada ya uhaba wa pesa kuchochea hasira na ukosoaji wa wananchi kabla ya uchaguzi wa Rais na Bunge baadaye mwezi huu.
-
Uchaguzi wa Nigeria: Jeshi lakanusha madai ya njama ya mapinduzi kabla ya uchaguzi
Feb 13, 2023 07:55Jeshi la Nigeria limekanusha madai ya chama tawala kwamba linapanga kuvuruga uchaguzi ujao wa rais nchini humo
-
IMN: Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yamekuwa na taathira kubwa kwa watu wa Nigeria
Feb 08, 2023 22:51Mmoja kati ya viongozi wa ngazi ya juu wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria (IMN) amesema kuwa Mapinduzi ya Kiislamu yya Iran yameleta matumaini kote ulimwenguni.
-
Watu 40 wauawa katika mapigano jimboni Katsina, Nigeria
Feb 04, 2023 03:56Watu zaidi ya 40 wameuawa katika mapigano baina ya kundi la wabeba silaha na wanakijiji waliojitolea kulinda usalama katika jimbo la Katsina, kaskazini mwa Nigeria.
-
Tume ya haki za binadamu ya Nigeria kulichunguza jeshi kuhusu madai ya utoaji mimba
Feb 01, 2023 23:34Tume ya haki za binadamu ya Nigeria imeteua jopo maalumu ambalo jukumu lake litajumuisha kuchunguza ripoti ya Reuters kwamba jeshi liliendesha mpango wa siri wa uavyaji mimba katika mapambano yake dhidi ya makundi yenye silaha kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
-
Mripuko wa bomu waua makumi ya watu katikati ya Nigeria
Jan 26, 2023 23:12Wafugaji 27 wa kabila la Fulani wamepoteza maisha huku wengine wengi wakijeruhiwa, baada ya bomu kuwaripukia katika kijiji cha Rukubi, katika mpaka wa majimbo ya Nasarawa na Benue, katikati ya Nigeria.
-
Mkutano wa ahadi wa kusaidia Bonde la Ziwa Chad umeanza nchini Niger
Jan 24, 2023 03:40Serikali za Niger, Ujerumani na Norway, pamoja na Umoja wa Mataifa zinashiriki kwa pamoja mkutano wa tatu wa ngazi ya juu kuhusu Kanda ya Bonde la Ziwa Chad, ambao ulianza jana na kuendelea leo katika kituo cha mikutano cha kimataifa cha Mahatma Gandhi katika mji mkuu wa Niger, Niamey.
-
Waislamu wa Nigeria wakosoa uchochezi wa jarida la Kifaransa
Jan 07, 2023 06:55Waislamu nchini Nigeria wamelaani kitendo cha dharau, kejeli na udhalilishaji cha jarida la Ufaransa la Charlie Hebdo cha kuchapisha vibonzo vya kumvunjia heshima Ayatullah Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Ajali mbili za barabarani zaua watu 21 Nigeria
Dec 28, 2022 08:02Polisi ya Nigeria imetangaza kuwa, watu 21 wamefariki dunia kutokana na ajali mbili za barabarani zilizotokea nchini humo siku ya Jumatatu na Jumanne.
-
Magaidi wa Boko Haram waua raia 17 kaskazini mwa Nigeria
Dec 27, 2022 04:07Vyombo vya habari vya Nigeria vimetangaza kuwa, watu 17 wameuawa kaskazini mashariki mwa nchi hiyo kufuatia shambulio lililofanywa na magaidi wa kundi la Boko Haram.