-
Hujuma dhidi ya Harakati ya Kiislamu Nigeria zimewafanya mayatima watoto 1,800
Jul 25, 2021 06:56Jukwaa la Akademia la Harakati ya Kiislamu ya Nigeria (IMN) limesema hatua ya vyombo vya usalama vya nchi hiyo kuhujumu na kushambulia shughuli za kidini za harakati hiyo imepelekea watoto karibu elfu mbili kuwa mayatima.
-
Wanakijiji 100 waliokuwa wametekwa nyara Nigeria waachiliwa huru
Jul 21, 2021 03:22Polisi ya Nigeria imesema, wanakijiji 100 wa eneo la kaskazini magharibi mwa nchi hiyo waliokuwa wametekwa nyara na magenge ya wabeba silaha wameachiwa huru baada ya mazungumzo iliyofanya na watekaji nyara hao waliokuwa wakiwashikilia watu hao kwa siku 42.
-
Rais Rouhani ataka kuimarishwa ushirikiano na Nigeria katika nyanja za kimataifa
Jul 20, 2021 03:40Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa wito wa kuimarishwa zaidi ushirikiano wa Tehran na Abuja.
-
Watu 45 wauawa na magaidi wenye silaha katika mji wa Faru, Nigeria
Jul 10, 2021 03:08Kundi la wanamgambo wenye silaha limeshambulia mji wa Faru wa kaskazini magharibi mwa Nigeria na kuua kwa akali watu 45 na kuwajeruhi makumi ya wengine.
-
Nigeria: Watu wenye silaha wameteka nyara wanafunzi 140 katika jimbo la Kaduna
Jul 05, 2021 22:04Kundi moja la wanamgambo wenye silaha limewateka nyara wanafunzi 140 katika shambulio lililofanya katika shule moja ya sekondari katika jimbo la Kaduna, huko kaskazini magharibi mwa Nigeria usiku wa kuamkia Jumapili iliyopita.
-
Makumi wa wanachama wa Boko Harama waangamizwa na jeshi la Nigeria
Jul 03, 2021 08:09Jeshi la Nigeria limetangaza habari ya kuangamiza makumi ya magaidi wa kundi la kigaidi la Boko Haram katika jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa nchi.
-
Kuakhirishwa kesi ya Sheikh Zakzaky na njama za mabeberu nchini Nigeria
Jul 03, 2021 06:22Mahakama ya Nigeria kwa mara nyingine tena imeakhirisha kikao cha kusikilizwa kesi ya kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria (IMN), Sheikh Ibrahim Zakzaky hadi tarehe 28 Julai licha ya Waislamu wa nchi hiyo kutaka mwanazuoni huyo aachiwe huru.
-
Kesi ya Sheikh Ibrahim Zakzaky yapigwa tarehe tena nchini Nigeria
Jul 02, 2021 02:13Mahakama ya Nigeria imeipiga tena tarehe kesi ya kiongozi wa Harakati ya Kisilamu ya Nigeria, Sheikh Ibrahim Zakzaky hadi mwishoni mwa mwezi huu wa Julai.
-
Wabeba silaha 14 waliojaribu kushambulia kituo cha polisi Nigeria wauawa
Jun 20, 2021 22:22Polisi nchini Nigeria imefanikiwa kuangamiza wabeba silaha 14 waliojaribu kuvamia kituo kimoja cha polisi katika jimbo la Benue, la katikati mwa nchi.
-
Wanafunzi wengine zaidi ya 80 watekwa nyara nchini Nigeria
Jun 18, 2021 03:32Zaidi ya wanafunzi 80 wa Nigeria wametekwa nyara katika shambulizi la watu waliokuwa na silaha huko Kaskazini Magharibi mwa Nigeria.